Na Vero Ignatus, Arusha

Naibu waziri wa Habarui, sanaa utamaduni na michezo Mhe. Juliana Shonza  amewataka wasanii wa Injili kjijengea tabia ya kujiwekea akiba ili punde wapatapo matatizo waweze kuyatatua kwa urahisi.

Ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akizindua mfuko wa Tagoane LoanFund Jijini Arusha ambapo amepongeza uongozi wa Tagoane kufikia hatua hiyo. Ameyataka mashirikisho yote ya muziki wa Injili nchini Tanzania kuiga mfano nzuri wa Tagoane ili waweze kuwa na mashirikisho ambayo ni hai na yanayoleta mshindo kwenye jamii.

Amesema yeye kama mlezi wa wasanii wote nchi amewaomba waamke wachangamkie fursa na wasiwe wavivu kujifunza kutoka kwa wenzao waliofanikiwa .Amewataka wasanii kukaa kwa pamoja Kuonyeshe Uzalendo kwa nchi yao wajadili changamoto mbalimbali wanazozipitia na kutafuta namna ya kutazua changamoto zinazowakabili.

Kwa upande wake Rais wa Tagoane Taifa Dkt. Godwin Maimu amesema kuwa wanedhamiria kuanzisha mfuko wao wa Tagoane Loan Fund ambapo mpaka sasa umekuwa na wanachama ambao wameshachangia akiba zao zipatazo shilingi milioni kumi.Amesema mfuko huo unatarajiwa kuanza kutoa mikopo kwa wanachama wavhqngiaji kuanzia 2 januari 2019

maendeleo kama vijana hayawezi kuendelea ukiwa na jitihada za mtu mmoja mmoja bali balintunapounganisha nguvu zetu kwa pamoja mwisho wa siku tunapata kitu cha kuweza kutusaidia. Alisema Dkt Maimu

Naibu waziri wa Habari, sanaa utamaduni na michezo, Juliana Shonza akizungumza katika tamasha Tukuza Festival Genesis one katika hotem ya Corido Spring Jijini Arusha. Picha/habari na Vero Ignatus.
Naibu Waziri wa Habari, sanaa, Utamaduni na michezo Juliana Shonza akipeana mikono na Rais wa Tagoane Dkt. Godwin Maimu mara baada ya kuzindua mfuko wa Tagoane Loan Fund Jijini Arusha.
Rais wa Mtandao wa wasanii wa Injili na Maadili Tanzania Dkt. Godwin Maimu akizungumza na wasanii mbalimbali waliohudhuria katika tamasha la Tukuza festival Genesis one Jijini Arusha.
Naibu waziri wa Habari sanaa utamaduni na michezo Juliana Shonza akisalimiana na Mkurugenzi wa Newlife Band Fortunatus Mabondo(Hondo)
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, utamaduni na michezo akipokelewa na kikundi cha ngoma cha jamii ya wamasai cha Meserani Jijini Arusha.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...