Na Amisa Mussa

MKUU  wa  Mkoa  wa  Tabora  Aggrey Mwanri ameahidi kuwashughulikia wataalam wa afya wanaowatoza fedha  wajawazito wakati kutaka kujifungua.

 Pamoja na mambo mengine amesema kwa sasa wanaendelea kuboresha upatikanaji wa huduma za afya pamoja na kupunguza vifo vya mama na mtoto mkoani humo.

Akizungumza katika kampeni za  Bima ya Afya ya Jamii(CHF) iliyoboreshwa pamoja na Kampeni ya  Jiongeze Tuwavushe salama ,Mwanri ametumia kampeni hizo kuwanyooshea vidole baadhi ya watoa huduma za afya ambao wanawatoza fedha wanawake wajazito wanakwenda kujifungua katika vituo vya afya na zahanati.

Mwanri amesema hatosita kumchukulia hatua za kinidhamu mtumishi wa afya atakayebainika kumtoza fedha mama mjamzito.

Katika hatua nyingine Mwanri ametoa onyo kwa wakurugenzi wa  Halmashauri  za  Wilaya  mkoani humo ambao  wamezembea  kuwasajili  wazee  na  kufungua  madirisha  maalum ya  kuwahudumia  katika hospitali  na zahanati zilizopo kwenye maeneo yao.

Kuhusu uzinduzi  wa  kampeni  hizo  imekwenda  pamoja na  Serikali ya  Mkoa  wa  Tabora  kupokea  magari  madogo  nanne ya kubeba wagonjwa kutoka Shirika  Care  International kupitia  mradi  wa  Tamani yenye  thamani  ya zaidi ya Sh.Milioni 184.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...