Serikali ya awamu ya Tano chini ya Mh Rais Dr.John Pombe Magufuli imeweka mipango madhubuti ya kuboresha huduma na mazingira katika makundi mbalimbali ya watu wenye ulemavu likiwemo kubwa la uwezeshwaji kiuchumi kupitia asilimia 2% ya mapato ya ndani ya Halmashauri na Manispaa nchini.

Hayo yamesemwa jana katika Hotel ya Hyatt Regency na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde kwa niaba ya Mh Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa Majaliwa wakati wa uzinduzi wa Taasisi ya HAJI MANARA FOUNDATION* ambapo Mavunde alitumia nafasi hiyo kuelezea mipango Serikali katika kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata fursa sawa katika masuala ya siasa,kijamii na ushiriki katika ustawi na ujenzi wa Taifa Tanzania.

Mavunde alichukua fursa hiyo kumpongeza sana Mwanzilishi wa Taasisi hiyo Ndg Haji Manara kwa uamuzi na utayari kusaidia watu wenye mahitaji na kuahidi kwamba Serikali itatoa kila ushirikiano kwa Taasisi hiyo katika kutimiza majukumu yake hasa katika kutoa elimu kwa jamii juu ya nafasi ya watu wenye ulemavu katika Jamii.

Akizungumza katika hafla hiyo,Ndg Haji Manara ambaye pia jana alizindua perfume yake iendayo kwa jina la De La Boss,amesema Taasisi hiyo ni itasaidia kuwajengea uwezo watu wenye Ualbino pamoja na kutoa elimu kwa jamii kuepukana na dhana potofu juu ya watu wenye ualbino,ambapo pia alibainisha kwamba

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,Mh Paul Makonda ametumia nafasi hiyo kumpongeza Haji Manara kwa ubunifu mkubwa na kuitaka jamii kuwaunga mkono watu wanaoleta mabadiliko na fikra mpya na sio kuwavunja moyo kwa majungu na maneno yasiyofaa.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde kwa niaba ya Mh Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa Majaliwa akimpongeza Haji Manara kwa kuzindua taasisi yake ya HAJI MANARA FOUNDATION pamoja manukato 'perfume' yake iliojulikana kwa jina  la De La Boss
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde kwa niaba ya Mh Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa Majaliwa akizungumza jamo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kushuhudia uzinduzi wa taasisi ya HAJI MANARA FOUNDATION pamoja manukato 'perfume' yake iliojulikana kwa jina la De La Boss,iliofanyika jana jijini Dar
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana na Ajira Mh Anthony Mavunde kwa niaba ya Mh Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa akiizindua manukato 'perfume' ya De La Boss mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika ukumbini humo kushuhudia tukio hilo lililofanyika jana jijini Dar.
Sehemu ya Meza kuu ikifurahia jambo
Msanii nyota wa Bongofleva almaarufu Diamond Platnumz akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa taasisi ya HAJI MANARA FOUNDATION pamoja manukato 'perfume' yake iliojulikana kwa jina la De La Boss,ambapoo viongozi mbalimbali wa serikali na wadau walihuduhuria tukio hilo adhimu kabisa.
Haji Manara akilishwa keki wakati wa uzinduzi wa taasisi ya HAJI MANARA FOUNDATION pamoja manukato 'perfume' yake iliojulikana kwa jina la la De La Boss,ambapoo viongozi mbalimbali wa serikali na wadau walihuduhuria tukio hilo adhimu kabisa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...