Selina Mushi wa Mlandizi Njia Panda JKT anasikitika kutangaza kifo cha mume wake mpendwa Clement Thomas Ndeleokasi Shayo  kilichotokea Alhamsi tarehe 29, Novemba 2018 katika hospitali ya Muhimbili - Mloganzila. 


Mazishi yalifanyika nyumbani kwa marehemu, Uparo-Kirua Vunjo Moshi, Kilimanjaro siku ya Jumanne tarehe 4 Desemba, 2018. Watoto wa marehemu, Frederick Clement Shayo na Regina Clement Shayo, pamoja na mama yao Selina Mushi na dada wa marehemu Clementina Thomas Shayo  wakishirkiana na famlia ya Mtika na ukoo wote wa Shayo, pamoja na familia ya Lesiaki Mushi wanatoa shukrani za dhati kwa wauguzi wa hospitali ya Muhimbili-Mloganzila kwa juhudi zao za kujaribu kuokoa maisha ya mpendwa wao Clement. 

Shukrani zao za pekee zinatolewa kwa Sista Agatha wa kituo cha Afya cha Mtakatifu Joseph, Luguruni Dar es Salaam, ndugu, jamaa na marafiki wote waliomhudumia Clement wakati wa kuugua kwake.  Marehemu aliugua akalazwa hospitali kwa muda mfupi na kuruhusiwa; kisha akapata stroke.  

 Kifo cha Clement kimekuwa mshtuko mkubwa kwa ndugu, jamaa, marafiki, na wote waliomfahamu Tanzania, Marekani na Canada. Bwana Ametoa na Bwana Ametwaa, Jina Lake Lihimidiwe. Mwenyezi Mungu aipokee roho ya marehemu Clement katika Furaha ya Milele, Amina

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Rest In Peace Mr Shayo! Poleni sana familia yake na ndugu na jamaa wote.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...