Mwenyekiti wa bodi ya wakaguzi akiwa amesimama na baadhi ya wajumbe wa bodi kujadili maendeleo mazuri ya ujenzi unaoendelea katika eneo hilo la lemuguru kata ya kisongo,nakupewa maelekezo na Mratibu wa mradi wa ujenzi Mhandisi Peter Kagady
Mwenyekiti wa bodi ya wakaguzi nchini mhandisi Alexander kyaruzi(Alievaa miwani) akipewa muongozo wa ujenzi utakaoendelea katika eneo hilo la legumuru kata ya kisongo na mratibu wa mradi mhandisi peter kigadya( alievaa koti la langi ya chungwa) mbele ya wajumbe ya bodi
Mwenyekiti wa bodi ya wakaguzi nchini Mhandisi alexander kyaruzi kati kati akikakagua moja ya mashimo yanguzo aliochimbwa kwaajili ya kusimamisha minara mikubwa ya umeme.
Baadhi ya vijana wanaojishughurisha na ujenzi wa upandishwaji wa nguzo kubwa za umeme wilayani monduli , ikiwa ni moja ya mradi unaondelea katika njia za usambazaji wa umeme vijijini.
Mwenyekiti wa bodi ya ukaguzi nchini Mhandisi Alexander Kyaruzi pamoja na wajumbe wa bodi ya ukaguzi wakijadilianana kupeana maelekezo pamoja na waratibu wa ujenzi wa kituo cha kupooza na kusambasa umeme lemuguru kata ya kisongo mkoani arusha.
Eneo la ujenzi utakaofanyika wa kupooza na usambazaji umeme uliopo lemuguru kata ya kisongo mkoani arusha ambapo magari yanabeba udongo usiofaa kwa ujenzi na kuweka udongo unaofa kwa ujenzi




Na. Vero Ignatus Arusha


Mwenyekiti wa bodi ya Tanesco nchini Mhandishi Alexander Kyaruzi kwa kushirikiana na wajumbe wa bodi hiyo wamefanya ukaguzi katika kituo kikubwa cha kupoza na kusambaza umeme uliopo Lemguru Kata ya Kisongo mkoani Arusha

Akizungumza wakati walipotembelea mradi huo Mhandisi Kyaruzi amesema lengo la ziara hiyo ni kujionea maendeleo, hali ya usimamizi ya miradi, ambapo hadi sasa vipo vituo viwili ambacho cha Lemguru wanaongeza kilovet 400 - 420 eneo lingine linaloboreshwa ni kutoka Iringa mpaka Shinyanga lenye msongo wa kilovet 400 

Kwa mujibu wa Mhandisi Kyaruzi mradi huo mkubwa wa kupooza na kusambaza umeme unaunganisha nchi za Zambia, Kenya, Uganda na wenyeji Tanzania, ambapo utaweza kuleta uhakika wa umeme unatokea katika mikondo mbali mbali ya maji,kama vile Uganda unatumia mto ambao unasambaza umeme katika nchi nyingine za Africa ikiwemo Tanzania

Aidha Mhandisi Alexander Kyaruzi amefurahishwa, na kuwapongeza wasimamizi wa mradi huo kwa juhudi zinazofanywa,katika kusimamia vyema pamoja na kuwapa vijana nafasi za ajira katika maeneo hayo huku akiwatakaa kuzidisha kasi ya uendeshaji wa mradi hadi kufikia mwaka 2020

‘‘Tulivyo kuja hapa kwanza tulifurahi pamoja na kwamba ni mwanzo na kwenye mwanzo mzuri unaoneka,lakini hapa tunaona wanaondoa kwanza udongo na kubadilisha udongo ambao haufai kwa ujenzi na kuweka udongo kwa ajili ya ujenzi ndipo waaanze ujenzi maana ujenzi huu wa mradi tumeweka mikakati mpaka mwaka ujao uwe umekamilika,na ukitoka hapa unaelekea Singida mpaka Namanga’’ Alisema

Alisema mradi unategemea mpaka kufikia mwaka 2020 uwe umekamilika na mradi utaleta faida za umeme katika vijiji vyote nchini,na pia utaleta manufaa kwa vijana wasio na ajira na wanaokaa vijiweni kupata fursa za ajira

Hata hivyo mratibu wa mradi wa njia za kusafirisha umeme wa msongo wa kilovet 400 Afrika ya Mashariki katika nchi za Zambia,Kenya,Uganda na Tanzania Mhandisi Peter Kigadya amesema mpaka sasa maendeleo ya mradi yamefikia pazuri na mradi umeunganishwa kutokea Kenya mpaka Arusha na kuelekea Singida.

Amesema mradi mzima wa una sehemu kubwa tatu ujenzi wa njia za umeme na njia kuu za kupoozea umeme,pamoja na usafirishaji wa umeme katika vijiji,sehemu ya kwanza kwanza Iinatoka Singida mpaka babati,na sehemu ya pili ni babati mpaka arusha, na sehemu ya tatu arusha mpaka namanga na njia zote tatu zipo katika ujenzi na mpaka sasa njia hizo wameziwekea msingi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...