Katibu Mkuu Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo
akijibu akizungumza na waraghabishi kutoka mikoa mbalimbali katika
mkutano wa Digitali kwa maendeleo ulioandaliwa na Shirika la
OxfamTanzani na kufanyika Katika ukumbi wa African Dreams Jijini Dodoma
Naibu waziri wa Elimu William Olenasha akizungumza katika mkutano wa Waraghabishi wa Digitali kwa Maendeleo ulioandaliwa na Shirika la. OXFAM Tanzani Jijini Dodoma
Naibu
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia na Mbunge wa Ngorongoro William
Olenasha akipita taarifa kupitia simu yake ya mkononi katika mkutano wa
Digitali kwa Maendeleo ulioandaliwa na Shirika la Oxfam Jijini Dodoma
Sabore Ngarusi
Kutoka wilayani Ngorongoro akiuliza swali kwa Katibu Mkuu wizara ya
Maji Profesa Kitila Mkumbo kwamba wizara hiyo imejipangaje kuondoa taizo
la maji wilayani humo.
Mbunge wa Viti maalum Dodoma Mhe. Fatuma Tawfiq akifuatilia mjadala katika mkutano huo wa Digitali kwa Maendeleo Jijini Dodoma
Mbunge wa Mbogwe mkoa wa Geita Mhe. Maselle akifuatilia mjadala kwa makini
Mbunge
wa Mtwara vijijini Mhe. Hawa Ghasia akichangia mjadala katika Mkutano
wa Digitali kwa Maendeleo ulioandaliwa na Shirika la Oxfam Nchini Jijini
Dodoma
Mbunge wa Viti maalum Dodoma Mhe. Fatuma Tawfiq akichangia mada katika mkutano huo wa Digitali kwa Maendeleo Jijini Dodoma
Katibu mkuu Wizara ya maji Profesa Kitila Mkumbo akifuatilia mjadala Digitali kwa Maendeleo kwa makini Jijini Dodoma
Jimmy Luhende Kutoka Shirika la ADLG. akichangia mada katika mkutano wa waraghabishi wa Digital Kwa maendeleo ulioandaliwa na Shirika la Oxfam Tanzania.
Naibu Waziri wa Elimu Williwm Olenasha akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi kutoka katika Shirika la Oxfam Tanzania
Naibu
waziri wa Elimu Willium Tate Ollenasha akiwa katika picha ya pamoja na
viongozi mbalimbali na Waandishi wa habari za mtandaoni Jijini Dodoma
katika Mkutano wawaraghabishi Digitali kwa maendeleo
Na. Vero Ignatus, Dodoma
Zaidi
ya 30% ya miradi ya maji iliyokamilika vijijini haifanyi kazi kwasababu
imekabidhiwa kwa jamii kwani ni tofailuti na ile ya mijini ambayo
inakabidhiwa kwa Wahandisi au kwa wataalamu wa maji
Hayo
yamesemwa na Katibu mkuu Wizara ya Maji Profesa Kitila Mkumbo alipokuwa
katika mkutano wa waraghabishi Digitali kwa maendeleo Jijini Dodoma
ulioandaliwa na Shirika la Oxfam Nchini ambapo amesema miradi hiyo
inapokabidhiwa kwa wananchi haina uangalizi wa kutosha
Profesa
Mkumbo amesema Kituo kimoja Cha maji kinapaswa kuhudumia watu 250 hadi
kufikia January 2019 tayari wameshajenga vituo 130,000 vijijini na
vinavyofanya kazi,83,000 takribani wananchi 60 mpaka 65 wanapata maji.
Amesema
kuwa Madhumuni ya Sheria Mpya ya Rasilimali za Maji Na. 11/2009 ni
kuhakikisha kuwa Rasilimali za Maji hapa nchini zinatunzwa, zinatumiwa,
zinaendelezwa, zinaboreshwa, zinasimamiwa na kudhibitiwa kwa kuzingatia
kanuni
Amesema
kuwa Sheria mpya ya Maji iliyo pitishwa inagusia vipengele viwili
uanzishwaji wa wakala wa maji vijijini adhabu kwa watu wanao haribu
miundombinu ya maji
Amezitaja
Wilaya ya Ngorongoro iliyopo mkoani Arusha kuwa ni mojawapo yenye
changamoto kubwa ya kufikiwa kutokana na Jiografia yake ila hadi sasa
(Mb)Mh.William Ollenasha Ameshafanya usanifu vijiji 8 vitanufaika na
mradi wa maji
Akijibu
swali lililoulizwa na mmoja wa Waraghabishi kuhisiana na uondoshwaji
wa bei za maji Profesa Mkumbo amesema Mchakato wa kupandisha bei ya maji
ni shiriki, linaanza na mamlaka ya maji na mara nyingi upandaji wa bei
ya maji inategemeana na gharama za uendeshwaji wa mamlaka za maji
Vilevile
ameainisha Takwimu za upatikanaji wa maji kwamba zinazipata kwa aina
mbili ambazo ni Miundombinu ya maji ilivyo sambazwa, Kutumia water
system kwenye mtandao wa EWURA ambapo Tafiti yake hufanyika kwa
kuwapigia wananchi na kuwauliza maswali
'' Kwa mujibu wa Takwimu za mwaka 2017 za NBS zinaonesha 66% ya wananchi wa Tanzania wanapata maji'' Alisema Mkumbo
Kwa upande wake Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Yeknolojia na mbunge wa Ngorongoro Willium Olenasha amelishukuru Shirika la Oxfam kwa kutoa mafunzo kwa wananchi namna ya kutumia nyenzo za digitali ili kuleta maendeleo kwa jamii inayowazunguka.
Naibu
Waziri wa wa Elimu, Sayansi na Teknolojia William Olenasha amesema kuwa
Serikali ipo pamoja na Oxfam pamoja na Waraghabishi katika kuhakikisha
kwamba changamoto zinazoibuliwa na wananchi zinatatuliwa na viongozi
husika kwa haraka na kwa wakati.
Ameongeza
kuwa Nchi nyingi zimesonga mbele kwa kasi kwa sababu ya kutumia
teknolojia ya dijitali hivyo Oxfam imekua ikishirikiana na serikali
katika shughuli za maendeleo ikiwemo mradi huo wa Dijitali Kwa Maendeleo
Wakishukuru
Shirika la Oxfam kwa mafunzo ya kutumia nyenzo za Digitali kwa
maendeleo Lucy Samweli, Diwani viti Maalumu Kata ya Nyasato Geita
amesema Kwa kutumia mitandao ya kijamii amepata ushauri kutoka kwa watu
mbalimbali wanaosoma anachokituma katika mitandao hiyo na hivyo
kuboresha utendaji kazi yake
Na
Bi Royce Jumanne, Mraghabishi kutoka Kigoma amesema kuwa Kupitia simu
zao za mkononi waraghabishi wamefanikiwa kuhamasisha jamii kuchangia
madawati ili kuwezesha wanafunzi kusoma katika mazingira mazuri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...