Wadau mbalimbali wa uzalishaji wa mvinyo hapa nchini pamoja na
watumiaji wa kinywaji hicho wanatarajia kufurahia pamoja Siku ya
wapendanao yaani Valentine Day katika hafla ya maalum inayofahamika kama
‘Mkeka na Mvinyo’ itakayofanyika usiku wa Februari 14 katika hoteli ya
Whitesands jijini Dar es Salaam.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mratibu wa hafla hiyo kutoka kampuni ya Real PR Solutions (RPR), Bi Calorine Kirwanda amesema mbali na kuwakutanisha wadau muhimu wa kinywaji hicho, hafla hiyo inalenga kutoa fursa kwa watumiaji wa mvinyo hapa nchini kufurahia vinywaji tofauti vya aina hiyo vinavyozalishwa hapa nchini huku wakiwa wamekaa kwenye mikeka.
“Pamoja na kutoa fursa kwa watumiaji wa mvinyo siku hiyo kufurahia pamoja na wapendwa wao, usiku wa Mkeka na Mvinyo unalenga kuunga mkono jitihada za serikali katika kutangaza utalii na kukuza viwanda vya ndani kupitia uhamasishaji wa matumizi ya bidhaa zinazozalishwa hapa nchini ikiwemo aina tofauti ya mvinyo bora kabisa unaozalishwa hapa nchini,’’
“Upekee wa hafla hii unaanzia kwenye jina lake ‘ Mkeka na Mvinyo’. Hivyo basi itahusisha matumizi ya mikeka ambapo wageni wetu watapata fursa ya kuketi kwenye mikeka huku wakifurahi mvinyo bora unaozalishwa hapa nchini pamoja na nyama choma kadili ya matakwa yao,’’ alisema.
Aliwataja baadhi ya wadau muhimu katika kufanikisha hafla hiyo kuwa ni pamoja na Hoteli ya Whitesands, Bodi ya Utalii Tanzania, (TTB), GS 1, pamoja na kampuni ya magazeti ya TSN wazalishaji wa magazeti ya Daily News pamoja na Habari Leo.
Bi Kirwanda aliongeza kuwa hafla hiyo ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo utakaozinduliwa hivi karibuni unaolenga kutangaza utalii wa ndani pamoja kuvumbua fursa mbalimbali za kibiashara ndani ya nchini kwa lengo la kukuza uchumi unaofahamika kwa jina la ‘Domestic Tourism Promotion Initiative’ (DTPI).
“Tunahitaji kuhamasisha zaidi matumizi ya bidhaa za ndani ili kukuza uchumi wetu kama taifa,’’ aliongeza bi Kirwanda huku akitaja baadhi ya maeneo ambayo tiketi za hafla hiyo zinapatikana kuwa ni pamoja na Hoteli ya Whitesands na Shamo Tower Mbezi Beach.
Alisema, tofauti na mtu mmoja mmoja au kwa wale ambao watakuwa na wapendwa wao, Mkeka na Mvinyo inatoa fursa kwa mashirika na taasisi mbalimbali kufurahia pamoja katika dhana nzima ya kuonesha upendo, shukrani na pongezi baina yao na wadau wao katika shughuli zao za kila siku huku wakifurahia mvinyo na chakula kizuri katika viunga vya hoteli ya Whitesands.
“Ifahamike kwamba siku ya wapendanao sio kwa ajili ya wale wenye mahusiano ya kimapenzi tu bali pia inaweza kutumiwa na mashirika au taasisi mbalimbali lengo likiwa ni kuonesha upendo, shukrani na pongezi kwa wafanyakazi, na wadau mbalimbali wanaoshirikiana nao katika shughuli zao za kila siku,’’ alifafanua.
Akizungumza kwenye hafla hiyo Meneja Mauzo na Masoko wa kampuni ya magazeti ya TSN, Januarius Maganga alisema kampuni hiyo imeaamua kuunga mkono mpango huo kutokana na kuguswa kwake na namna unavyolenga kuchochea harakati za masoko kwa bidhaa za ndani sambamba na kuunga mkono agenda ya serikali ya uchumi wa viwanda.
Kwa upande wake Afisa Uhusiano Mwandamizi kutoka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bw Geofrey Tengeneza alisema kupitia mpango huo mbali na kutangaza utalii wa fukwe pia utatangaza utalii wa asili kwa kuwa utahusisha mvinyo unaozalishwa hapa nchini huku watumiaji wakiwa wameketi kwenye mikeka ya asili.

Afisa Uhusiano wa kampuni ya GS 1, Bi Clementine Kahamba (kushoto) akizungumza kuhusiana na hafla hiyo. akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na hafla hiyo itakayohusisha adau mbalimbali wa uzalishaji wa mvinyo hapa nchini pamoja na watumiaji wa kinywaji hicho itakayofanyika siku ya wapendanao yaani Valentine Day Februari 14 katika hoteli ya Whitesands jijini Dar es Salaam. Wengine ni pamoja na Mratibu wa hafla hiyo kutoka kampuni ya Real PR Solutions (RPR), Bi Calorine Kirwanda (wa pili kushoto), Meneja Mauzo na Masoko wa kampuni ya magazeti ya TSN, Januarius Maganga (wa pili kulia), pamoja na Meneja Uendeshaji wa Hotel ya Whitesands Bw Ali Hilika.
Mratibu wa hafla ya ‘Mkeka na Mvinyo’ kutoka kampuni ya Real PR Solutions (RPR), Bi Calorine Kirwanda (wa pili kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na hafla hiyo itakayohusisha adau mbalimbali wa uzalishaji wa mvinyo hapa nchini pamoja na watumiaji wa kinywaji hicho itakayofanyika siku ya wapendanao yaani Valentine Day Februari 14 katika hoteli ya Whitesands jijini Dar es Salaam. Wengine ni pamoja na Meneja Mauzo na Masoko wa kampuni ya magazeti ya TSN, Januarius Maganga (wa pili kulia), Afisa Uhusiano wa kampuni ya GS 1, Bi Clementine Kahamba (kushoto) pamoja na Meneja Uendeshaji wa Hotel ya Whitesands Bw Ali Hilika.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Mratibu wa hafla hiyo kutoka kampuni ya Real PR Solutions (RPR), Bi Calorine Kirwanda amesema mbali na kuwakutanisha wadau muhimu wa kinywaji hicho, hafla hiyo inalenga kutoa fursa kwa watumiaji wa mvinyo hapa nchini kufurahia vinywaji tofauti vya aina hiyo vinavyozalishwa hapa nchini huku wakiwa wamekaa kwenye mikeka.
“Pamoja na kutoa fursa kwa watumiaji wa mvinyo siku hiyo kufurahia pamoja na wapendwa wao, usiku wa Mkeka na Mvinyo unalenga kuunga mkono jitihada za serikali katika kutangaza utalii na kukuza viwanda vya ndani kupitia uhamasishaji wa matumizi ya bidhaa zinazozalishwa hapa nchini ikiwemo aina tofauti ya mvinyo bora kabisa unaozalishwa hapa nchini,’’
“Upekee wa hafla hii unaanzia kwenye jina lake ‘ Mkeka na Mvinyo’. Hivyo basi itahusisha matumizi ya mikeka ambapo wageni wetu watapata fursa ya kuketi kwenye mikeka huku wakifurahi mvinyo bora unaozalishwa hapa nchini pamoja na nyama choma kadili ya matakwa yao,’’ alisema.
Aliwataja baadhi ya wadau muhimu katika kufanikisha hafla hiyo kuwa ni pamoja na Hoteli ya Whitesands, Bodi ya Utalii Tanzania, (TTB), GS 1, pamoja na kampuni ya magazeti ya TSN wazalishaji wa magazeti ya Daily News pamoja na Habari Leo.
Bi Kirwanda aliongeza kuwa hafla hiyo ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo utakaozinduliwa hivi karibuni unaolenga kutangaza utalii wa ndani pamoja kuvumbua fursa mbalimbali za kibiashara ndani ya nchini kwa lengo la kukuza uchumi unaofahamika kwa jina la ‘Domestic Tourism Promotion Initiative’ (DTPI).
“Tunahitaji kuhamasisha zaidi matumizi ya bidhaa za ndani ili kukuza uchumi wetu kama taifa,’’ aliongeza bi Kirwanda huku akitaja baadhi ya maeneo ambayo tiketi za hafla hiyo zinapatikana kuwa ni pamoja na Hoteli ya Whitesands na Shamo Tower Mbezi Beach.
Alisema, tofauti na mtu mmoja mmoja au kwa wale ambao watakuwa na wapendwa wao, Mkeka na Mvinyo inatoa fursa kwa mashirika na taasisi mbalimbali kufurahia pamoja katika dhana nzima ya kuonesha upendo, shukrani na pongezi baina yao na wadau wao katika shughuli zao za kila siku huku wakifurahia mvinyo na chakula kizuri katika viunga vya hoteli ya Whitesands.
“Ifahamike kwamba siku ya wapendanao sio kwa ajili ya wale wenye mahusiano ya kimapenzi tu bali pia inaweza kutumiwa na mashirika au taasisi mbalimbali lengo likiwa ni kuonesha upendo, shukrani na pongezi kwa wafanyakazi, na wadau mbalimbali wanaoshirikiana nao katika shughuli zao za kila siku,’’ alifafanua.
Akizungumza kwenye hafla hiyo Meneja Mauzo na Masoko wa kampuni ya magazeti ya TSN, Januarius Maganga alisema kampuni hiyo imeaamua kuunga mkono mpango huo kutokana na kuguswa kwake na namna unavyolenga kuchochea harakati za masoko kwa bidhaa za ndani sambamba na kuunga mkono agenda ya serikali ya uchumi wa viwanda.
Kwa upande wake Afisa Uhusiano Mwandamizi kutoka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Bw Geofrey Tengeneza alisema kupitia mpango huo mbali na kutangaza utalii wa fukwe pia utatangaza utalii wa asili kwa kuwa utahusisha mvinyo unaozalishwa hapa nchini huku watumiaji wakiwa wameketi kwenye mikeka ya asili.
Afisa Uhusiano wa kampuni ya GS 1, Bi Clementine Kahamba (kushoto) akizungumza kuhusiana na hafla hiyo. akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na hafla hiyo itakayohusisha adau mbalimbali wa uzalishaji wa mvinyo hapa nchini pamoja na watumiaji wa kinywaji hicho itakayofanyika siku ya wapendanao yaani Valentine Day Februari 14 katika hoteli ya Whitesands jijini Dar es Salaam. Wengine ni pamoja na Mratibu wa hafla hiyo kutoka kampuni ya Real PR Solutions (RPR), Bi Calorine Kirwanda (wa pili kushoto), Meneja Mauzo na Masoko wa kampuni ya magazeti ya TSN, Januarius Maganga (wa pili kulia), pamoja na Meneja Uendeshaji wa Hotel ya Whitesands Bw Ali Hilika.
Mratibu wa hafla ya ‘Mkeka na Mvinyo’ kutoka kampuni ya Real PR Solutions (RPR), Bi Calorine Kirwanda (wa pili kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na hafla hiyo itakayohusisha adau mbalimbali wa uzalishaji wa mvinyo hapa nchini pamoja na watumiaji wa kinywaji hicho itakayofanyika siku ya wapendanao yaani Valentine Day Februari 14 katika hoteli ya Whitesands jijini Dar es Salaam. Wengine ni pamoja na Meneja Mauzo na Masoko wa kampuni ya magazeti ya TSN, Januarius Maganga (wa pili kulia), Afisa Uhusiano wa kampuni ya GS 1, Bi Clementine Kahamba (kushoto) pamoja na Meneja Uendeshaji wa Hotel ya Whitesands Bw Ali Hilika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...