Na Amisa Mussa
Mahakama Ya Hakimu  Mkazi  Mkoa  Wa  Tabora  Imemuhukumu  Kutumikia  Kifungo  Cha Miaka  Miwili Jela Au  Kulipa Faini Ya  Shilingi  Laki  Tano  Raia  Wa Ethiopia  Anayefahamika  Kwa  Jina  La  Gashahuni  Degu  Mwenye  Umri  Wa Miaka 21 Baada  Ya Kupatikana  Na Hatia  Ya  Kuingia  Nchini  Bila Kibali  Halali Kinyume  Cha  Sheria  Ya Uhamiaji  Sura  Ya 54 Iliyofanyiwa  Marejeo  Mwaka 2016.
Mwendesha  Mashitaka  Upande  Wa  Idara Ya Uhamiaji  Octavian  Kilatu Akisoma  Maelezo  Ya  Kosa Ameieleza  Mahakama Kuwa  Mtuhumiwa  Gashahuni  Alikamatwa Tarehe 21 Februari  Mwaka  Huu  Stend Kuu Ya Mabasi  Mjini  Tabora  Akisafiri  Kutoka  Mkoani  Mara  Kuelekea Mbeya  Hadi  Afrika  Ya  Kusini  Mahali  Ambako Alieleza  Alikuwa Anakwenda Kutafuta  Ajira.
Aidha Kutokana Na Hukumu Iliyotolewa  Na Hakimu  Mkazi  Mkoa  Wa  Tabora  Jocktan Rushwela  Ilifanya  Raia  Huyo  Wa Kigeni  Gashahuni  Degu  Kuangua   Kilio Hadharani  Katika  Viwanja  Vya  Mahakama  Akidai  Kuomba  Msamaha.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...