Na Amisa
Mussa
Mahakama Ya
Hakimu Mkazi Mkoa
Wa Tabora Imemuhukumu
Kutumikia Kifungo Cha Miaka
Miwili Jela Au Kulipa Faini
Ya Shilingi Laki
Tano Raia Wa Ethiopia
Anayefahamika Kwa Jina
La Gashahuni Degu
Mwenye Umri Wa Miaka 21 Baada Ya Kupatikana
Na Hatia Ya Kuingia
Nchini Bila Kibali Halali Kinyume Cha
Sheria Ya Uhamiaji Sura
Ya 54 Iliyofanyiwa Marejeo Mwaka 2016.
Mwendesha Mashitaka
Upande Wa Idara Ya Uhamiaji Octavian
Kilatu Akisoma Maelezo Ya
Kosa Ameieleza Mahakama Kuwa Mtuhumiwa
Gashahuni Alikamatwa Tarehe 21
Februari Mwaka Huu
Stend Kuu Ya Mabasi Mjini Tabora Akisafiri
Kutoka Mkoani Mara
Kuelekea Mbeya Hadi Afrika
Ya Kusini Mahali
Ambako Alieleza Alikuwa Anakwenda
Kutafuta Ajira.
Aidha
Kutokana Na Hukumu Iliyotolewa Na
Hakimu Mkazi Mkoa
Wa Tabora Jocktan Rushwela Ilifanya
Raia Huyo Wa Kigeni
Gashahuni Degu Kuangua
Kilio Hadharani Katika Viwanja
Vya Mahakama Akidai
Kuomba Msamaha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...