Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii.

Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson amesema aliyekuwa Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Vipindi Ruge Mutahaba aliyefariki Jana usiku nchini Afrika Kusini ametimiza yake katika uibuaji wa mawazo na kuwa na Matokeo chanya.

Dkt Tulia ameyasema hayo wakati alipokwenda kutoa pole nyumbani kwa marehemu Ruge mikocheni jijini Dar es Salaam.Amesema kuwa ni pigo kuondekewa na Ruge kwa familia pamoja na Taifa katika kutoa mchango wake kwa mawazo.

Aidha amesema kuwa wakati wa uhai wake Ruge akianzisha jambo alikuwa haileweki lakini kadri ya muda kwenda watu wanaanza kujua kuhusiana na kitu alichokianzisha."Kazi ya Mungu haina makosa ila Ruge tutaendelea kumkumbuka daima na Milele kwa mchango wake kwa vijana nchini".Amesema Dkt.Tulia Amesema kuwa msiba wa Ruge sio wa Tanzania bali Dunia nzima kutokana na yeye kufahamika kwa kazi anayoifanya.
Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson akizungumza na baadhi ya vyombo vya habari mapema leo nyumbani kwa marehemu Ruge Mutahaba,Mikocheni jijini Dar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...