Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka
ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Deusdedit C.V Kakoko
anasikitika kutangaza kifo cha Baba yake mzazi, Mzee Conatus Vitalis Kakoko
(81) kilichotokea juzi katika Hospitali ya Agakhan alipokuwa amelazwa kwa
takribani wiki moja akisumbuliwa na maradhi ya Ini na Figo.
Hadi umauti unamkuta, Mzee
Conatus Vitalis Kakoko ameacha watoto wanne (4) na wajukuu kumi na tano (15).
Misa ya kumuaga marehemu Mzee
Conatus Vitalis Kakoko itafanyika katika kanisa la MT. Petrol lililopo
Oysterbay siku ya Jumatatu, tarehe 11/2/2019 saa tatu asubuhi.
Mara baada ya misa hiyo,
mwili wa marehemu Mzee Conatus Vitalis Kakoko utasafirishwa, ambapo Mazishi yatafanyika siku ya Jumatato
tarehe 13/02/2019 kijijini kwake, Munjebwe, Rulenge mkoani.
Bwana Ametoa na Bwana
Ametwaa. Jina lake litukuzwe.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...