Na Karama Kenyunko
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imesema Februari 21, mwaka huu itamsomea maelezo ya awali (PH) msanii wa Filamu nchini, Wema Sepetu anayekabiliwa na shtaka moja la kuchapisha video ya ngono na kusambaza katika mitandaoni ya kijamii.
Hatua hiyo imefikiwa leo Februari 13, 2019 baada ya Wakili wa Serikali, Glori Mwenda kuieleza mahakama kuwa, upelelezi wa shauri hilo umekamilika na kuimba mahakama kupanga tarehe ya kumsomea mshtakiwa huyo PH.
Kufuatia taarifa hiyo Hakimu Mkazi, Maira Kasonde, ameiahirisha kesi hiyo mpaka Februari 21, mwaka huu.
Wema ambaye alikuwa Miss Tanzania mwaka 2006,
anatetewa na Wakili, Ruben Simwanza, alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Novemba Mosi, 2018, kujibu shtaka hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...