Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Medicana , Bursa ya nchini Uturuki Prof. Serdar Ener akisoma taarifa ya mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji wa moyo na kulazwa katika chumba cha wagonjwa waliopo katika uangalizi maalum (ICU) alipotembelea Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo wanazotoa na kuona namna wanavyoweza kufanya kazi kwa pamoja ya kutoa matibabu ya moyo kwa watanzania.
Afisa Muuguzi bingwa kutoa Connecticut Children’s Medical Center nchini Marekani ambaye yupo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kujitolea kuwafundisha wauguzi jinsi ya kuwahudumia wagonjwa waliolazwa katika chumba cha uangalizi maalum (ICU) Mollie Mullaney akiongea jambo na Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Medicana , Bursa ya nchini Uturuki Prof. Serdar Ener. Prof. Ener alitembelea Taasisi hiyo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo wanazozitoa ikiwa ni pamoja na kuangalia miondombinu iliyopo.
Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Medicana , Bursa ya nchini Uturuki Prof. Serdar Ener akiangalia jinsi madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wanavyofanya upasuaji alipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo wanazozifanya na kuona namna wanavyoweza kufanya kazi kwa pamoja ya kutoa matibabu ya moyo kwa watanzania.
Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Medicana , Bursa ya nchini Uturuki Prof. Serdar Ener akiangalia jinsi madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wanavyofanya upasuaji alipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo wanazozifanya na kuona namna wanavyoweza kufanya kazi kwa pamoja ya kutoa matibabu ya moyo kwa watanzania.
Afisa Muuguzi wa chumba cha upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Faustina Mwapinga akimweleza jinsi wanavyoandaa vifaa vya upasuaji Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Medicana , Bursa ya nchini Uturuki Prof. Serdar Ener alipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo wnazozitoa ikiwa ni pamoja na kuangalia miondombinu iliyopo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiongea jambo na Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Medicana , Bursa ya nchini Uturuki Prof. Serdar Ener alipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo wanazozitoa na kuona namna wanavyoweza kufanya kazi kwa pamoja ya kutoa matibabu ya moyo kwa watanzania.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akiwa katika picha ya pamoja na Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo kutoka Hospitali ya Medicana , Bursa ya nchini Uturuki Prof. Serdar Ener pamoja na wageni wengine kutoka nchini humo mara baada ya kumalizika kwa ziara yake ya kutembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuangalia huduma za matibabu ya moyo wanazozifanya na kuangalia miundombinu iliyopo. Picha na JKCI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...