Na: Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.

Jumla ya viwanda 3,504 vimeanzishwa nchini kutokana na juhudi za kujenga uchumi wa viwanda zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano tangu iingie madarakani hadi kufikia Desemba, 2018.

Hayo yameelezwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Chumbageni, Mhe. Ussi Salum Pondeza juu ya viwanda vingapi vimeanzishwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda.

"Kati ya viwanda hivyo 3,504 vilivyoanzishwa, vinajumuisha viwanda vidogo sana 2,500, viwanda vidogo 943, viwanda vya kati 51 na viwanda vikubwa 10," amesema Mhandisi Manyanya.

Amesema wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina imekuwa ikifanya tathmini ya viwanda 156 vilivyobinafsishwa na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa kwa viwanda 68 ambavyo havijaendelezwa.

Aidha amesema, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilijiridhisha na mapendekezo yaliyotolewa na kuiwezeshsa Ofisi ya Msajili wa Hazina kuchukuwa hatua.

Mhandisi Manyanya amesema hatua iliyochukuliwa na Ofisi ya Msajili ni kuvirejesha viwanda 14 Serikalini na juhudi za kuvitafutia wawekezaji wengine walio tayari kuviendeleza zinaendelea.

Ameeleza kuwa, kwa mujibu wa hali ya uchumi ya mwaka 2017, mchango wa sekta ya viwanda katika Pato la Taifa ni asilimia 5.5 ikilinganishwa na asilimia 4.9 mwaka 2016, sawa na ongezeko la asilimia 0.6.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...