Jumla ya  wanafunzi 52  wa stashahada ya ualimu kutoka katika chuo cha ualimu cha Monduli wamefika   katika ofisi za  Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania, Makao Makuu Njiro Arusha  kwa lengo la kujifunza kwa vitendo masuala mbali mbali ya kisayansi ambayo wamekuwa wakiyasoma katika nadharia.

Lengo la ziara hii ya siku moja kwa wanafunzi hawa ni kujifunza ili kufahamu dhana nzima ya juu ya matumizi salama ya mionzi na namna udhibiti unavyofanyika na wao kuwa mabalozi wazuri katika uhamasishaji wa matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania Profesa Lazaro Busagala amewaeleza wanafunzi hao kuwa elimu waliyoipata katika ziara hii ya mafunzo itawawezesha kuelewa matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia na kujilinda na mionzi pindi watakapokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kikazi hapo baadaye.

Kiongozi wa wanafunzi hao Mwalimu  Sikana Menard ameeleza kuwa ziara hiyo imewasaidia wanafunzi hao ambao ni walimu watarajiwa hapo baadae katika masomo ya sayansi kuwa wamepata  elimu kubwa kuhusiana na masuala ya mionzi.

Amesema wamekuwa wakiwafundisha wananfunzi kwa njia ya nadharia tu hivyo kwa kutembelea kwenye Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania kutawasaidia sana kujionea teknolojia mbali mbali katika maabara za TAEC zenye ubora wa hali ya juu kwa ajili ya mafunzo.

Aidha TAEC inaendelea kuwakaribisha wananchi, wanafunzi na wadau mbalimbali ili kujipatia elimu na kujifunza masuala tofauti tofauti yanayohusu udhibiti salama wa mionzi na  matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia  hapa nchini.

Imetolewa na;


Peter G. Ngamilo
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...