Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile ametembelea Taasisi ya Tiba ya mifupa, upasuaji wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu (MOI)kukagua maendeleo ya chumba maalum cha Tiba mtandao ambacho kinatarajia kukamilika na kufanya kazi kuanzia mwezi Juni mwaka huu.

Awali akiwa kwenye taasisi hiyo ya MOI, Dkt. Ndugulile aliweza kupokea maendeleo ya ukamilishwaji wa chumba hicho cha tiba mtandao ambapo pia aliwataka kuhakikisha wanasimamia vizuri  uendeshaji wake  kwani utasaidia Taifa kutoa huduma za kibingwa sehemu kubwa zaidi hapa nchini zikiwemo hospitali za rufaa za mikoa na nyingine

Aidha, Dkt. Ndugulile amewataka kukamilisha hatua zote za chumba hicho na kitakapokamilika  uzinduzi ufanyike kama inavyotarajiwa

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Dkt. Respicious Boniface amesema kuwa, chumba hicho kinategemea kukamilika na kuanza kufanya kazi mwezi  Juni mwaka huu na kitakapokamilika kitasaidia matibabu kwa kwa njia ya mtandao nchi nzima

“Chumba cha Tiba mtandao hapa MOI kitakapokamilika hospitali zote kubwa za rufaa za mikoa na zingine za  Rufaa, zitatuma picha hapa na watalaam wa MOI wanatoa majibu na kurudisha tiba kule na kutoa ushauri wa jinsi wa kutoa matibabu kwa wagonjwa wakiwa hukohuko” alieleza Dkt. Boniface.

Chumba hicho cha tiba  mtandao kinatarajiwa kuwepo kwenye jengo jipya la MOI ambapo tayari timu ya watalaam wanaendelea na taratibu za kukamilisha uendeshaji wake.

MOI ni miongoni mwa Taasisi za tiba zenye kutoa huduma za kibingwa huku ikiwa na Madaktari wabobezi kwenye tiba ya mifupa, upasuaji wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu.

 Naibu Waziri Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile (Mb) ametembelea kituo Cha Utafiti na Maabara ya ugonjwa wa Seli Mundu kilichopo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Wakati akiwa katika ziara hiyo, aliwasisitiza watalaam kuhakikisha maabara hizo zinakuwa na manufaa mapana kwa wananchi  ambao mara nyingi wanachelewa kujua kama wanamatatizo ya Seli Mundu na magonjwa mengine ya kurithi. Aidha, alieleza maabara hiyo ni miongoni mwa maabara chache sana Africa Mashariki hivyo, zitumike vyema  kupata matokeo chanya pamoja na kutumika kujifunza na kufanyia tafiti mbalimbali kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...