Na Said Mwishehe,Globu ya jamii.


KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe pamoja na mwanachma mwenye kadi namba moja wa Chama hicho Maalim Seif Sharif Hamad wameendelea kuchanja mbuga ikiwa ni mkakati wa kuzungumza na wanachama wao. 

Maalim Seif aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi(CUF)amejiunga na ACT -Wazalendo baada ya kutoridhika na uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam baada ya kumtambua Profesa Ibrahim Lipumba katika nafasi ya uenyekiti wa CUF.

Wakizungumza kwenye mahojiano maalum yaliyofanyika jijini Dar es Salaam Maalim Seif na Zitto wamekiri mkakati wa wao wa kuwa pamoja si wa kukurupa bali yamefanyika mazungumzo ya kutosha yaliyokwenda sambamba na kufanyika kwa utafiti kabla ya kufikia uamuzi.

Kwa upande wake Maalim Seif amesema kutokana na mgogoro uliokuwa ndani ya CUF yeye pamoja na viongozi wenzake walianza kuweka mipango mipya ambayo itawawezesha kuendelea na siasa.Moja ya mkakati ulikuwa ni kutafuta Chama ambacho ambacho watajiunga nacho , hivyo wamejirisha kuwa ACT- Wazalendo ndio sehemu sahihi kwao.

"Kujiunga na ACT haikuwa jambo la kukurupuka , tumetafakari, tumefanya uchunguzi na tumejiridhisha tuko sehemu sahihi na mapambano yanaendelea.Wakati tukiendelea na kesi tuliamua kuanza kujiandaa kwa kutafuta Chama sahihi ambacho kitatufaa.Hivyo ujio wetu ACT ni maandalizi ya muda mrefu,"amesema Maalim Seif.

Kuhusu tuhuma za kwamba Maalim Seif ni Mamluki wa CCM, amejibu kuwa tuhuma hizo zimekuwa zikielekezwa kwake kwa muda mrefu lakini hajawahi kuzijibu kwani anajua anachokifanya.

"Ningekuwa mamluki usingetengezwa mgogoro CUF ili kutudhoofisha kisiasa na hakari za kudai demokrasia huru nchini. Sababu za mgogoro ulipo ndani ya CUF ni kupunguza nguvu yangu ya kisiasa. Nipo ACT kuendeleza mapambano ya kisiasa ili kuipata Tanzania mpya,"amesema Maalim Seif.

Alipoulizwa anatoa kauli gani baada ya baadhi ya wanachama aliiondoka nao CUF kuonekana wakiwa wameshika vitabu vitakatifu wakati wanapandisha bendereza ACT visiwani Pemba, amejibu hakuna udini wowote.

"Kutaka jina la Mwenyezi Mungu katika shughuli za kila siku kwa jamii ya Watanzania ni mambo ya kawaida.Ndio maana hata Bungeni kabla Bunge kuaza dua inayoambatana na kutajwa kwa jina la Mungu ni jambo la kawaida.Hivyo sioni kosa lilipo,"amesema Maalim Seif.

Hivyo amefafanua hakuna mambo ya udini ila kilichotokea wanachama hao waliamua kusema Alhau Akibarr kwa maana ya Mungu Mkubwa na ni jambo la kawaida.

Kwa upande wake Zitto amesema kitendo cha Maalim Seif kujinga na ACT-Wazalendo kunafungua ukurasa mpya na Maalim Seif ameandika historia mpya huku naye akitumia nafasi hiyo kueleza ujio wake ndani ya chama hicho mchakato wake ulianza muda mrefu.

"Tulikuwa tunaangalia namna ambavyo wenzetu CUF mgogoro wao unavyoendelea, tukaona ACT ni jukumu letu kuhakikisha tunajiandaa ili wenzetu wakikosa nafasi tunaungana nao na kuendelea na mapambano katika medani za kisiasa. Maandalizi ya Maalim Seif kuja kwetu hayakuwa maandalizi ya muda mfupi bali ni ya muda mrefu.Tunawapokea pia watu ambao wanapenda mabadiliko na wamechoka kuburuzwa,"amesema Zitto.

Akizungumzia tuhuma za kwamba Zitto ni mamluki, amejibu kuwa "Kwanza nieleze tu historia ya miaka michache imeonesha dhahiri kuwa maneno ya umamluki si sahihi na Watanzania wanaona namna ambavyo chama ninachokiongoza kilivyokuwa mwiba.

"Pili kiongozi lazima awe na uwezo wa kuunganisha watu, ukiona kiongozi anagawa watu basi uongozi wake una mashaka, hivyo kwake aliona iwapo kuna fursa ya kuunganisha watu. Muhimu ni matendo na huwezi kuzuia watu wasiseme.Wakati nagombana na Chadema nilikuwa na nafasi ya kwenda CCM lakini niliona hakuna sababu hiyo kwani lengo ni kuendeleza mapambano.Siwezi kuwa mamluki,"amesema Zitto.

Wakati huo huo, jana Maalim Seif pamoja na Zitto walikuwa visiwani Zanzibar wakizungumza na wanachama na wapenzi wa ACT na leo wameendelea kuchanja mbuga kwani wapo mkoani Tanga.ACT-Wazalendo wameamua kumtambulisha Maalim Seif kwa wanachama wao huyo ambaye amekwenda huko akiwa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa CUF ambao wanamuunga mkono Maalim.
KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe akiwa pamoja na Maalim Seif aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi(CUF)amejiunga na ACT -Wazalendo 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...