*Ahoji kuhusu Mahakama ya mafisadi, ahoji kuhusu jina hilo la Mahakama  mafisadi ni nani katika mahakama hiyo, je ni majaji? Mawakili? Washtakiwa au mashahidi? apendekeza jina hilo kubadilishwa

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
JAJI mkuu mstaafu na Mkuu wa Chuo kikuu cha Mzumbe Barnabas Sammata ameshauri kubadilishwa kwa jina la mahakama ya mafisadi na litafutwe jina ambalo litasadifu wanaopelekwa katika mahakama hiyo ni washtakiwa.

Akizungumza katika mdahalo uliowakutanisha na wanafunzi wa chuo cha sheria nchini na kujadili mada kuhusiana na mapambano dhidi ya rushwa katika utoaji wa huduma ya mahakama jaji Sammata amesema kuwa jina la mahakama ya mafisadi halisadifu wanaopelekwa katika mahakama hiyo kwa kuwa haifamiki mafisadi ni akina nani?, majaji? Mawakili? au mashahidi? na akashauri jina mbadala litafutwe ili kusadifu wanaopelekwa katika mahakama hiyo.

Katika mdahalo huo jaji Sammata alitoa rai kwa wanasheria kote nchini kuwa mstari wa mbele kupinga kansa ya rushwa wakati wa utoaji wa huduma kwa wananchi.
Jaji Mkuu mstaafu na Mkuu wa chuo kikuu cha Mzumbe Barnabas Sammata akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha sheria nchini katika mdahalo wa uwajibikaji na mapambano dhidi ya rushwa katika utoaji wa huduma ya haki na mahakama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...