Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Mhe. Augustino Mrema(kushoto) akiongoza Kikao cha 40 cha kujadili Wafungwa waliopendekezwa kunufaika/kutonufaika katika mpango wa Parole. Kulia ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Kamishna wa Magereza, Uwesu Ngarama ambaye pia ni Kaimu Katibu wa Sekretarieti ya Bodi ya Taifa ya Parole. Kikao hicho cha siku moja kimefanyika leo Machi 8, 2019, katika Bwalo la Maafisa Magereza, lililopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
PIX 2
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Kamishna wa Magereza, Uwesu Ngarama ambaye pia ni Kaimu Katibu wa Sekretarieti ya Bodi ya Taifa ya Parole akitoa taarifa fupi ya Sekretarieti kabla ya kumkaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Mhe. Augustino Mrema(hayupo pichani)afungue rasmi kikao hicho.
PIX 3
Wajumbe wa Bodi ya Taifa ya Parole wakifuatilia majadiliano ya wafungwa waliopendekezwa kunufaika/kutonufaika katika mpango wa Parole leo Machi 8, 2019, katika Bwalo la Maafisa Magereza, lililopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam.
PIX 4
Ujumbe kutoka Zanzibar wakishiriki mazungumzo maalum yenye lengo la kubadilishana uzoefu na Bodi ya Taifa ya Parole Tanzania katika ziara yao ya kikazi leo Machi 8, 2019. Wa kwanza kushoto ni Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Said Hassan(katikati) ni Waziri wa TAMISEMI na Vikosi Maalum vya Zanzibar, Mhe. Haji Omari na Kulia ni Kamishna Msaidizi wa Polisi kutoka Zanzibar, Hasina Ramadhani.
PIX 5
Sekretarieti wakifuatilia kwa makini majadiliano katika kikao hicho.
PIX 6
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole, Mhe. Augustino Mrema(wa nne toka kushoto walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Taifa ya Parole pamoja na Viongozi Waandamizi kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, leo Machi 8, 2019, katika Bwalo la Maafisa Magereza, lililopo Ukonga, Jijini Dar es Salaam baada ya ufunguzi wa Kikao cha Bodi ya Taifa ya Parole(Picha zote na Jeshi la Magereza).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...