Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Dkt.Semistatus Mashimba amefanya ziara ya kutembelea baadhi ya shule za msingi za Chemba ikiwemo Songoro,Mapango na Chandama na kuangalia mazingira ya shule hizo ikiwemo kukagua taaluma na miundombinu ya shule hizo pamoja na changamoto wanazozikabili na namna ya kuzitatua,Pichani ni Mkurugenzi Dkt Mashimba akizungumza na baadhi ya Wafunzi wakati wa ziara yake.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya chemba Dkt.Semistatus Mashimba akipata maelezo kidogo kutoka kwa mmoja wa mafundi ujenzi alipotembelea na kufanya ukaguzi wa ujenzi unavyoendelea katika hospitali ya wilaya ya Chemba.Dkt Mashimba amefanya ziara kwenye moja wapo ya mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Chemba hatua kwa hatua,ambapo alieleza na kutoa maagizo kwa Wakandarasi kuwa ifikapo Machi 31/2019 majengo ya Chemba yote yawe yamefikia hatua ya renta
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...