UTANGULIZI


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inatangaza mafunzo katika Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi nchini Israel. Mafunzo hayo ni ya miezi 11 kuanzia mwezi Septemba, 2019 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Serikali ya Israel kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mafunzo hayo yatahusisha pia vitendo (field attachment) kwenye mashamba makubwa ya mazao mbali mbali yakiwemo ya matunda, mbogamboga, ufugaji, uvuvi na mazao mengine ya biashara kwa ujira maalum. 

SIFA NA VIGEZO VYA MWOMBAJI

      i.     Awe ni raia wa Tanzania mwenye umri wa kati ya miaka 20-35 pamoja na cheti cha            kuzaliwa na Kitambulisho cha Uraia.  
 ii.        Awe amehitimu mafunzo ya Kilimo katika ngazi ya shahada ya Chuo Kikuu,                         Stashahada au Astashahada ya Vyuo vya kilimo vinavyotambulika nchini. 
iii.        Awe na afya njema.  
iv.        Awe na ujuzi wa kuandika na kuongea lugha ya Kiingereza.   
 v.        Awe na uwezo wa kufanya kazi na watu wa tamaduni mbalimbali.  
vi.        Awe tayari kurejea nchini baada ya mafunzo yake.         

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...