Na, Editha Edward-Tabora
Mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Bilali Khamis (61) mkazi wa Mtaa wa Ushirika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora amekatwa sehemu zake za siri na Mpenzi wake Veronica Ngayawula baada ya Kutompa fedha ya sikukuu ya Pasaka hali iliyopelekea kufanyiwa ukatili huo wa kijinsia
Tukio hili la kikatili limetokea majira ya saa saba usiku wa kuamkia tarehe 22 mwaka huu nyumbani kwa Bilali Khamis
Juma Maswezi ambaye ni ndugu wa Bilali ameiambia Michuzi Blog kuwa kitendo alichofanyiwa ndugu yake siyo kitu kizuri kwani ni uzalilishaji ulio kinyume na haki za binadamu
George Mgalega ni Mganga Mkuu mfawidhi Hospitali ya Wilaya amesema kuwa amekili kumpokea mgonjwa huyo
"Baada ya kumfanyia uchunguzi tumegundua kwamba ametendewa kitendo hicho kwa kutumia kitu ncha kali kwa hiyo afya yake itachukua muda mrefu sana kuimalika maana kidonda hiki kimekaa wazi kwa muda mrefu"amesema Mgalega
Hata hivyo kwa matibabu na uchunguzi zaidi mzee Bilali amepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Nkiga Igunga huku Mpenzi wake Veronica Ngayawula akiwa ametokomea kusiko julikana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...