Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya imeendelea kuiunga mkono Serikali katika sera ya viwanda vya dawa kwa kutekeleza maelekezo ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuanzisha kiwanda cha kuzalisha maji tiba ‘Dripu’ za IV (Intravenous Fluids) kwa kutumia wataalamu wake wenye.

Dripu hizo zenye ujazo wa mil’s 250 na Mil’s 500 zimeanza kutumika kwaajili ya kuhudumia wagonjwa wenye uhitaji hali inayosababisha kuondokana na adha ya kununua\kuagiza dripu nje ya nchi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali Dkt Godlove Mbwanji amesema “Tunayo furaha kubwa kuanza uzalishaji wa maji tiba kwa ajili ya mahitaji ya hospitali yetu na kwa kufanya hivi, napenda kutoa shukrani nyingi kwa Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutuunga mkono na kutusaidia. Uko mpango wa kuhakikisha tunazalisha maji tiba kwa kiwango kikubwa ili kutoa huduma hiyo kwa wengine ukanda wa Nyanda za Juu Kusini”.

Amesema uanzishwaji wa kiwanda cha kutengeneza Maji Tiba (Dripu) umetekelezwa kwa kutumia mapato ya ndani na katika hatua inayofwata imeanza maandalizi ya mpango wa kutengeneza dawa ya macho.

Hadi sasa Hospitali ya Rufaa ya kanda Mbeya imeendelea kutoa huduma za kibingwa kwa kutumia vipimo vya kisasa kama Endoscopy, Digital X-Ray, ECG Ultra sound, Echo-cardiogram na siku za karibuni huduma ya CT Scan, Digital Radiography na Digital Mammography zitaanza kutolewa.
 Baadhi ya maji tiba Drip yanayozalishwa na Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya
 Muonekano wa maji tiba Drip

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...