Mjini Namtumbo, Mhe. Rais Magufuli amezindua Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) kilichojengwa na Serikali ya Tanzania kwa gharama ya shilingi Bilioni 6.5 na ambacho kitakuwa na uwezo wa kutoa mafunzo kwa wanafunzi 600 wa kozi ndefu na fupi kwa mwaka.
Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutoridhishwa kwake na gharama kubwa zilizotumika ikilinganishwa na thamani ya majengo yaliyojengwa na ameitaka VETA na viongozi wote wa Serikali kutambua umuhimu wa kubana matumizi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Mafunzo ya Ufundi, Mhe. Joyce Ndalichako amesema pamoja na chuo cha VETA Namtumbo, Serikali imejenga vyuo vingine vya VETA katika Mikoa ya Njombe, Rukwa, Geita na Simiyu. Pia imejenga vyuo vya maendeleo ya jamii 20 ambavyo vitaongezeka hadi kufikia 34 ifikapo mwaka 2020.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...