Naibu
waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhe, Mhandisi Atashasta Nditiye
afungua rasmi Baraza jipya la wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania -
TRC katika ukumbi wa Bandari jijini Dar es Salaam hivi karibuni Aprili
2019.
Hafla hiyo ya ufunguzi wa Baraza la wafanyakazi TRC kwa mara ya kwanza
tangu kuunganishwa kwa iliyokuwa Kampuni ya Reli Tanzania – TRL na Kampuni Hodhi ya Rasilimali za Reli – RAHCO na kuanzishwa TRC.
Baraza jipya la wafanyakazi lina jukumu la kusimamia na kutetea maslahi ya wafanyakazi kupitia wawakilishi kutoka idara na vitengo vya taasisi pamoja na wajumbe wa kamati tendaji wanaotokana na wajumbe wa baraza.
kulingana na katiba ya baraza na taratibu za kisheria Baraza lina kazi ya kupitia na kutoa maoni na kuboresha utendaji wa Shirika,pia baraza ni chombo cha kuleta upendo na umoja baina ya wafanyakazi.
Mgeni rasmi wa ufunguzi wa Baraza hilo naibu waziri Mhe. Atashasta Nditiye amelipongeza Shirika la Reli Tanzania kwa kufanya uamuzi huo wa kuundwa Baraza jipya na kuwataka wajumbe kulifanya Baraza kama sehemu wa kuwawakilisha wafanyakazi kwa lengo la kutatua matatizo changamoto na kuleta tija katika Shirika.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania - TRC alisema kuwa serikali inafuatilia Mali za Shirika ambazo zinamilikiwa na watu binafsi wamejibinafisha kwa njia zisizo halali na kuomba wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania kushirikiana katika kutoa taarifa sahihi ili rasilimali hizo zirudi kuongeza mapato kusaidia kuendesha Shirika ikiwemo kuinua maslahi ya wafanyakazi.
Naibu
waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhe, Mhandisi Atashasta Nditiye
akifungua rasmi Baraza jipya la wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania -
TRC katika ukumbi wa Bandari jijini Dar es Salaam hivi karibuni Aprili
2019.
Picha
tofauti za matukio katika Hafla ya ufunguzi wa Baraza la kwanza la
wafanyakazi TRC tangu kuunganishwa kwa kampuni mbili zilizokua TRC,yaani
Kampuni ya Reli Tanzania(TRL) na kampuni hodhi ya Reli (RAHCO)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...