Na Woinde Shizza Globu ya jamii

Msaada wa mabati 50 yenye thamani ya shilingi milioni 1.5 kwa shule ya
msingi ya Mkonoo ,ambayo iliezuliwa Marchi 30 mwaka huu kutokana na
mvua iliyoambatana na upepo.

Akikabidhi msaada huo jana kwa mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel
Dacqaro, Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni mornaban Dk Philemon Mollel,
aliesema akiwa ni mdau wa elimu ameguswa sana na tukio hilo la
kuezuliwa kwa paa la shule na hivyo ametoa mabati hayo ili kuharakisha
kuezekwa kwa vyumba vya madarasa na kuwezesha wanafunzi kuendelea na
masomo yao.

Amesema mara baada ya kupata taarifa hiyo amejitoa kuchangia mabati
hayo geji 28 kutokana na kutambua umuhimu wa elimu kwa wanafunzi hivyo msaada huo utawezesha madarasa hayo matatu kuezekwa kwa haraka.

Akipokea msaada huo mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqaro,
amempongeza mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo, Dakta Phileoni
Mollel, kwa moyo wake huo wa kujali wanafunzi .

Amesema serikali kwa upande wake itaendelera kushirikisha wadau
wengine wa maendeleo kutoa misaada ya vifaa vya jenzi ili kuwezesha
wanafunzi wanasoma kwenye mazingira mazuri na salama..

Aidha amesema katika tukio hilo pia shule ya sekondari Mkoo nayo
imeathiriwa na mvua hiyo na kuezuliwa paa kwenye chumba kimoja cha
maabara na baadhi ya nyumba zilizopo jirani na shule hiyo..Ameongeza kwamba licha ya msaada huo bado shule hizo zote mbili zina
uhitaji wa bati 90 za geji 28 .

Akipokea msaada huo kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel
Daqaro, mwalimu wa vifaa wa shule hiyo ya msingi Mkonoo,
mwalimu,Ndeningwalanga Kaaya, amesema shule hiyo ya msingi ina jumla
ya wanafunzi 990 kuanzia darasa la kwanza hadi la saba .

Ameongeza kuwa kutokana na tukio hilo wanafunzi wa darasa la saba
ambao wapo kwenye mikondo miwili wanalazimika kusomea chumba kimoja.
Mkuu wa wilaya ya Arusha GabrielDaqaro, akipokea msaada wa mabati hayo kutoka kwa Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni mornaban Dk Philemon Mollel
 Mkuu wa wilaya ya Arusha GabrielDaqaro, akipokea msaada wa mabati hayo kutoka kwa Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni mornaban Dk Philemon Mollel

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...