Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania TRC afungua mkutano wa mafunzo ya usalama katika uendeshaji wa shughuli za reli Kwa wafanyakazi wa Shirika la Reli Tanzania katika ukumbi wa mikutano wa bandari jijini Dar es Salaam.
Lengo la mafunzo hayo ni kuwakumbusha wafanyakazi wa reli kuimalisha ulinzi Na usalama wa binadamu Na miundombinu ya reli Kwa kutoa elimu ya usalama katika shughuli za uendeshaji wa reli Kwa madereva, wakaguzi wa reli, wahandisi mawasiliano, wahandisi mitambo, walinzi Na wabadilisha njia za reli.
Aidha, Mkurugenzi Mkuu Ndugu Kadogosa amesisitiza usalama wa reli unagusa maisha ya watu na kila mmoja ndani ya shirika Anawajibu wa kusimamia sheria Na kanuni zilizowekwa katika uendeshaji wa treni ili kuokoa maisha ya watanzania Na kutunza miundombinu ya reli,Aliendelea kusisitiza Mkurugenzi.
" tunaendelea Na ukarabati wa reli ya zamani kutoka Dar es Salaam Mpaka Isaka, tunategemea ndani ya mwaka mmoja ujao tutakuwa Na reli nzuri sana maana yake tusipokuwa Na umakini wa usalama tunaweza kusababisha ajari zikaongezeka Na Uharibifu kuwa mkubwa,"
Kwa upande wake kaimu mkuu wa kitengo cha usalama wa reli TRC Mhandisi Adolphina Ndyetabula amefafanua kuwepo Kwa elimu ya usalama ambayo hutolewa wa Shirika na wakazi wanaoishi maeneo ya reli ili kuzingatia swala Zima la usalama wao na miundombinu ya reli.


Mkurugenzi Mkuu shirika la Reli Tanzania Ndugu Masanja Kungu Kadogosa akitoa maelezo kwa wafanyakazi wa TRC kipindi cha ufunguzi wa mafunzo ya usalama katika uendeshaji wa shuguli za Reli katika ukumbi wa bandari hivi karibuni Aprili.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...