SHIRIKA la reli
nchini limewatoa hofu watanzania kuhusu umeme Utakao tumika katika shughuli zote za
kuendesha usafiri wa treni ya umeme
inayotarajiwa kuanza kazi zake za usafiri tokea
Dar es Salaam mpaka Morogoro kwa hatua ya kwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa mradi kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro Eng Ayubu
Mdachi alisema kuwa kukamilika kwa reli
hiyo kutaongeza pato kubwa kwa taifa.
Aidha amewataka
wananchi kuwa walinzi wakuu wa mradi huo kwani kuna watu wengine hawana
nia njema na maendeleo ya nchi yetu.
Aliongeza kuwa umeme
utakaotumika katika uendeshaji wa
treni hiyo ni wa hali ya juu kwani
kila mkoa utakuwa umeunganishwa hivyo
kama ikitokea kukatika kwa umeme Morogoro basi treni hiyo itatumia wa mkoa wa
pwani la sivyo ukatike nchini nzima
napo bado treni hiyo itafanya kazi zake kutokana na uwezo wake wa kutunza umeme yenyewe.
Kwa upande wake Edwini
Kalisa katibu wa baraza la wafanyakazi
la shirika la reli nchini alisema
kuwa serikali inasitahili pongezi za
dhati kutokana na hali halisi jinsi inavyoelekea katika nchini yetu kwani
mizigo itasafirishwa kwa urahisi na haraka kuliko Barabara za kupitia magari.
Aliongeza kuwa
usafirishaji wa treni ijayo ya umeme
itasaidia sana kwenye sekta ya viwanda kutokana na uwepo wa malighafi kutegemeana kutoka sehemu mbalimbali za mkoa.
Aidha katibu huyo aliongeza kuwa treni hiyo itakuwa ni ya kwanza barani Afrika kutokana na ubora wake unavyoonekana.
Katibu wa Baraza la Wafanyakazi la Shirika la reli nchini,Edwini Kalisa akizungumza leo na waandishi wa habari katika kituo cha soga mara baada ya kutembelea na kukagua jinsi mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa standard Gauge Soga mkoa Pwani.(Picha na Emmanule Massaka wa Mchuzi TV Dar es Salaam)
Meneja Msaidizi SGR kwa upande wa Shirika la Reli nchini(TRC), Mhandisi,Ayubu Mdachi, akizungumza na wafanyakazi la shirika la reli nchini namna mradi huo unavyoendelea katika Lot 1 inayotoka Dar es Salaam mpaka Morogoro.
wafanyakazi la shirika la reli nchini wakiangalia reli ya kisasa ya SGR kwenye eneo la Soga mkoa wa Pwani.
Picha ya pamoja
Ujenzi wa mradi wa reli SGR ukiendelea katika eneo la Stesheni jijini Dar es Salaam.Muonekano wa sehemu ya nguzo za mradi wa Standard Gauge. Sehemu ya reli ambayo imekamilika.Muonekano wa Stesheni ya Pugu ikiwa bado inaendela kujengwa. Mafundi Wakiendelea na Ujenzi wa Madaraja na kalavati katika eneo la mradi wa SGR.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...