Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa akitazama vifaa vya kisasa katika maabara ya nyuklia
Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa akitazama vifaa vya kisasa katika maabara ya nyuklia
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema Akizungumza
Mbunge wa Viti Maalumu Catherine Magige akizungumza

Wananchi wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa maabara
Picha ya pamoja ya Mgeni rasmi na kamati ya maandalizi
picha ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa pamoja na Wafanyakazi wa Tume ya mionzi.
picha ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa pamoja naViongozi wa Mkoa wa Arusha

Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa akitazama maabara ya Nyulia iliyozinduliwa katika tume ya Mionzi jijini Arusha.



Na Vero Ignatus, Arusha.

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amezindua maabara ya kisasa ya nyuklia iliko katika Time ya Mionzi Tanzania jijini Arusha ambapo maabara hiyo itasaidia kutumia nyuklia kwa ustawi wa jamii na maendeleo ya taifa.

Majaliwa amesema kuwa maabara hiyo ni muhimu katika kuhakikisha kuwa hakuna madhara yanayotokana na matumizi ya mionzi kwa kuwa na vifaa na wataalamu waliobobea katika mionzi.

Aidha amesema kuwa Tanzania ina hazina ya tank 58.2 za nyuklia katika maeneo mbalimbali ikiwemo Namtumbo,Nachingwea,Minjingu na Songea Vijijini."Maabara hii ya kisasa itasaidia kuongeza mchango wa nyuklia kwenye ustawi wa jamii na maendeleo ya taifa" Alisema Majaliwa

Naibu Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto Dr.Faustine Ndugulile ambaye alimuwakilisha Waziri wa Elimu na Sayansi na Teknolojia amesema kuwa maabara hiyo ya kisasa barani Afrika imejengwa kwa ushirikiano wa Jumuiya ya Umoja wa nchi za Ulaya na serikali ya Tanzania .

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema maabara hiyo itawawezesha Wataalu kudhibiti mionzi katika maeneo mbalimbali hususan viwanja vya ndege.

Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Atomiki Najat Mohammed ametaja majina ya Wafanyakazi bora ambao wamedhibiti vyanzo vya mionzi katika bidhaa na maeneo ya mipakani licha ya kushawishiwa na rushwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...