Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akipokelewa na Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai kabla ya kuanza kwa mechi ya mpira wa miguu kati ya timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliyochezwa leo katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mwenye Kijani ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Zubeir Ali Maulid, Mbunge Viti Maalum, Mhe. Salma Kikwete (wa pili kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Pastobas Katambi (katikati). Mechi hiyo iliisha kwa timu zote mbili kufunga magoli 2 -2, Lengo likiwa ni kuboresha uhusiano baina ya Mabunge hayo.
Wachezaji wa timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (kulia) wakisalimiana na Wachezaji wa timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kabla ya kuanza kwa mechi ya kirafiki baina yao iliyochezwa katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mechi hiyo iliisha kwa timu hizo kufungana magoli 2 -2, Lengo likiwa ni kuboresha uhusiano baina ya Mabunge hayo.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (kulia), Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia) wakifuatilia mechi kati ya timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliyochezwa leo katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Watatu kushoto ni Waziri Kiongozi Mstaafu wa Zanzibar, Mhe. Shamsi Vuai Nahodha na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Mhe. Pastobas Katambi.
Mbunge wa Kilolo, Mhe. Venance Mwamoto (katikati) ambae pia ni Kocha Mchezaji na Mfungaji wa bao la kwanza la timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akizungumza na Wachezaji wa timu ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa mapumziko katika mechi iliyowakutanisha timu hiyo na timu ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Mechi hiyo iliisha kwa timu hizo kufungana magoli 2 -2, Lengo likiwa ni kuboresha uhusiano baina ya Mabunge hayo.
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakishangilia goli walilofunga dhidi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar mchezo uliochezwa leo katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Kuanzia kushoto ni Mbunge wa Iringa Mjini, Mhe. Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Mafinga Mjini Mhe. Cosato Chumi na Mbunge wa Kilolo Mhe. Venance Mwamoto ambaye pia ni mfungaji wa goli hilo na nyuma ni Ndg. Onesmo lau lau. Katika mchezo huo timu hizo zilifungana magoli 2 -2, Lengo likiwa ni kuboresha uhusiano baina ya Mabunge hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...