Na Editha Edward-Michuzi TV Tabora 

Mkuu wa mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ametoa onyo kwa mtu atakaye haribu mazingira kwa njia ya ukataji wa miti hovyo.

Kauli hiyo ameisema wakati akishiriki zoezi la upandaji wa miti na wanafunzi wa chuo cha Teknolojia cha Dar es Salaam (D. I. T) katika kata ya kanyenye manispaa ya Tabora ikiwa ni juhudi za kuboresha Mazingira 

"Mtu atakayekamatwa anafanya Uharibifu wa Mazingira atasukumwa ndani, tunachofanya hapa ni kuotesha miti kila Halmashauri iwe na vitalu vyake kuanzia kwa mkuu wa Mkoa, mkuu wa Wilaya mtendaji wa kata, Mtendaji wa kijiji pamoja na Mtendaji wa mtaa, tunataka tuhakikishe miti hii inapandwa katika Taasisi zote"Amesema Mwanri

Aidha kiongozi wa Wanafunzi wa Chuo cha D. I. T Machage Emmanuel amesema Lengo la kushiriki zoezi hilo la upandaji wa miti ni kuimarisha Mazingira na kupata uhifadhi wa vyanzo vya maji na kuifanya Tabora kuwa ya kijani.
Pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri ambaye ameshiriki zoezi la upandaji wa miti pamoja na wanafunzi wa chuo cha D. I. T.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...