Makamu wa Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akipokelewa na mwenyeji wake,Balozi wa UAE,nchini Afrika Kusini Mahash Saeed Alhameli kabla ya kikao cha majadiliano ya ushirikiano baina ya ujumbe wa Bunge la Afrika na ujumbe kutoka Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE) jana Mei 5,2019 jijini Pretoria,Afrika Kusini.
Kushoto ni Makamu wa Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akizungumza tete-a-tete na Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE),nchini Afrika Kusini Mahash Saeed Alhameli.
Makamu wa Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akiongoza kikao cha majadiliano kuhusu ushirikiano wa bunge la Afrika na Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE) ambapo Ujumbe wa Bunge la UAE umeongozwa na Spika wa Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE), Dk. Amal Abdulla Al Qubaisi ,kwa pamoja wamekubaliana mambo ya msingi ya kushirikiana baina ya mabunge hayo.
Makamu wa Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akiagana na mwenyeji wake,Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu (United Arab Emirates- UAE),nchini Afrika Kusini Mahash Saeed Alhameli.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...