KANLESA wa nchini Ujerumani Angela Merkel ametunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima ya Chuo Kikuu maarufu cha Harvard.

Rais wa Chuo cha Havard Larry Bacow ambaye ndiye aliyemtunukia Merkel tuzo hiyo amesema kuwa Kansela huyo wa Ujerumani ni mwanasiasa mwenye nguvu barani Ulaya.

Wakati wa sherehe za kutunukiwa kwa Shahada hiyo ya Udaktari, chuo hicho kimemsifu Merkel kwa matamshi yake "Tutaweza kulisimamia hili" wakati wa mgogoro wa wakimbizi ulioanza mwaka 2015 nchini Ujerumani wakati aliporuhusu idadi kubwa ya wakimbizi na kukabiliwa na ukosoaji mkubwa nchini mwake.

Akizungumza kwenye hotuba yake kwa wanafunzi, wakati wa mahafali ya 368 ya chuo hicho cha Havard, Merkel amewaonya wanafunzi dhidi ya kuchanganyikiwa na kuuchukulia uongo kuwa ukweli na ukweli kuwa ni uongo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...