Mkurugenzi Mkuu wa Forum CC Rebecca Muna akizungumza leo kuhusu umuhimu wa wadau wa mazingira kuwa na jukwaa la pamoja la kujadiliana na kufikia makubakiano ya namna bora ya kukabiliana na changamoto zilizopo katika eneo la mazingira nchini.
Mchokoza mada Samuel Bubegwa akichangia wakati wa majadiliano ya wadau wa mazingira katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Dar es Salaam ambapo emetumia nafasi hiyo kushauri uwepo wa jukwaa la majadiliano ambalo litajikita kuweka mikakati ya kuondoa taka zikiwemo taka ngumu.
Ofisa Programu wa ForumCC Euphrasia Shayo akifuatilia majadiliano yaliyohusu mazingira ambayo yameandaliwa na ForumCC kwa kushirikiana na Halmashauri ya Ilala kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya(EU).
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omar Kumbilatomo akizungumza kwa niaba ya Meya wa manispaa hiyo akizungumza wakati akifungua kikao cha majadiliano kiichowakutanisha wadau wa mazingira na ForumCC.
Moja ya wadau wa mazingira Kahana Lukumbuzya akichangia mada wakati wa kikao cha majadiliano kuhusu uboreshaji wa mazingira ya Halmashauri ya Ilala jijini Dar es Salaam.
Wadau wa mazingira wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam wakifuatilia majadiliano yaliyohusu kuwekwa mikakati ya kuweka mazingira safi ya manispaa hiyo.
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
SHIRIKA la FORUMCC kwa kushirikiana na
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam wamewakutanisha wadau
mbalimbali kwa lengo la kujadili changamoto za kimazingira na kutafuta ufumbuzi
wake kwa hamashauri hiyo.
Mjadala huo unafanyika chini ya ufadhili wa
Umoja wa Ulaya(EU) kupitia Mradi wa Mazingira na Mabadiliko ya Tabianchi. EU
wamekuwa wakishirikiana kuandaa mijadala na makongamano yanayohusu kujadili
mabadiliko ya tabianchini na hali ya mazingira nchini kwa ujumla.
Akizungumza wakati wa akifungua majadiliano
hayo Meya wa Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam Omari Kumbilamoto amesema ni
jambo muhimu wadau kukutana na kuweka mikakati itakayosaidia kuweka mazingira
safi.
“Tunashukuru kwa uwepo wa majadiliano haya yanayohusisha
sekta binafsi na Serikali kwa kuangalia namna gani wanaweza kukabiliana na taka
ngumu.Mjadala umekuja wakati muafaka hasa kwa kuzingatia tayari Serikali imetoa
tamko la kuzuia plastiki ambalo binafsi na Halmashauri ya Ilala tunaunga mkono
katazo hilo,”amesema.
Amesema Manispaa ya Ilala imekuwa na jitihada
mbalimbali katika utunzaji mazingira kwa kuweka mbinu na mifumo sahihi za usafi
mazingira huku akisisitiza kutambua mchango wa sekta binafsi katika jitihada
hizo.
Pia ameshauri kampuni ambazo zipo Manispaa ya
Ilala na zinatoa huduma za kubeba taka ngumu pamoja na kufanya vizuri maeneo ya
kati ya Jiji ni vema pia wakaweka nguvu kubwa katika kuzoa taka maeneo ya
pembezoni.
“Ni lazima kuwepo na mipango madhubuti ya
kuzoa taka katika Manispaa ya Ilala.Pia niwakumbushe wenye kampuni za kuzoa
taka kuendelea kushirikiana na wananchi na vema nikaeleza gharama ya Sh.3000 ya
taka nayo inaonekana kuwa changamoto kwa wananchi walio wengi, hivyo mtaangalia
namna ya kufanya.
“Tunatarajia majadiliano ya leo yatakuwa na
ufumbuzi mzuri katika kumaliza changamoto za taka na kuweka mazingira safi
lakini nikiri bado tunayo changamoto ya dampo na kwa bahati nzuri wenzetu wa
Jiji wameahidi kutafuta ufumbuzi kwa kuwa na dampo la kisasa,”amesema
Kumbilamoto.
Pia amesema pamoja na Manispaa ya Ilala
kukusanya mapato mengi yatokanayo na vyanzo mbalimbali vya fedha lakini
ifahamike kuwa imekiwa ikitumia fedha nyingi kwa ajili ya masuala mbalimbali
yakiwamo ya sekta ya afya na kufafanua Ilala tayari imetenga Sh.milioni 52 kukabiliana
na Dengue na wakati huo huo kuna viashiria vya magonjwa ya mlipuko ,”amesema
Kumbilamoto.
Wakati wa majadiliano hayo imefafanuliwa
katika katika eneo la taka ngumu bado kunachangamoto kubwa na hivyo wadaua
wameamua kuweka mikakati ambayo itasaidia kuondoa taka hizo.Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa ForumCC
Rebecca Muna amesema lengo la kuwakutanisha wadau hao ni kuhakikisha kunakuwa
na makubaliano ya pamoja katika kukabiliana na changamoto ya uwepo wa taka
ngumu.
Amesema wanatambua dhamira njema ya Serikali ya
kuondoa taka hizo ikiwemo mifuko ya Plastiki, hivyo Forum CC kwa kushirikiana
na wadau wengine wa mazingira wanawajibu kuwa sehemu ya kufanikisha malengo ya
Serikali.
Pia
ametumia nafasi hiyo kusisitiza umuhimu wa uwajibikaji kwa kuhakikisha kila
mmoja wetu kwa maana ya Serikali, wadau na mtu mmoja moja anakuwa sehemu ya
kufanikisha mazingira yanakuwa salama.
“Forum CC ni shirika ambalo si la kiserikali
ambalo limekuwa likiandaa majadiliano yanayohusu mabadiliko ya tabianchi.Kwa
kuwa tunatambua tunaingia kwenye katazo la mifuko ya plastiki tukaona iko haja
ya kukutanisha wadau kuweka mikakati ambayo itsaidia kuondosha plastiki ambazo
zinachangia kwa kiasi kikubwa uchafuzi wa kimazingira,”amesema Muna.
Amefafanua uchafuzi wa mazingira una madhara
makubwa yakiwemo ya kutumia fedha nyingi kukabiliana na magonjwa ya mlipuko,
hivyo ni vema wadau wakaendelea kuweka mikakati ili kuhakikisha mazingira yanakuwa
safi,”amesema.
Hata hivyo amesema kuwa kikubwa ambacho
kinahitaji ni kuweka uwajibikaji ambao utakuwa na tija kwa kila mmoja
kutekeleza majukumu yao iwe kwa upande wa serikali au wadau wa mazingira.
Mmoja wa wachokozi wa mada Samuel Bubegwa
wakati akichangia majadiliano hayo amefafanua kwa Manispaa ya Ilala wamekuwa na
mfumo mzuri katika kuweka mfumo wa uzoaji taka na kuweka mazingira safi na
kuomba ni vema Ilala ikaangalia namna ya kukutana na viongozi wa ngazi za juu
serikalini ili kuwaelimisha namna wanavyofanya katika eneo la mazingira.
Pamoja na mambo mengine sehemu kubwa ya taka
ngumu zilikuwa zinatokana na plastiki na saas kuondolewa kutasaidia kimazingira
huku akishauri uwepo wa jukwaa kati ya wakandarasi, wadau na Serikali katika uondoshaji wa taka.
Ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa kwa
manispaa ya Ilala taka ambazo zinazalishwa kila siku ni tani 2000 na hivyo ni
jukumu la wadau mbalimbali kushirikiana katika kuondoa taka hizo na Ilala
imekuwa ikijitahidi katika kuweka mazingira safi.
Kwa upande wake Ofisa Mazingira Mkuu wa
Baraza la Mazingira la Taifa(NEMC) Mhandisi Benjamin Mchwampaka amesema suala
la uwepo wa uchafuzi wa mazingira linatokana na tabia na hivyo ni vema wananchi
wakabadili tabia.
Amesema kuna kila sababu ya taka kuwekwa
kulinana na aina ya taka zenyewe, ikiwemo taka zinazooza, taka ngumu pamoja na
taka zenye kemikali za sumu na kila familia ikiweza kutenganisha taka uwezekano
wa kudhibiti taka ngumu utafanikiiwa.
Mwisho


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...