Mkoa wa mtwara ukiwa ni mwenyeji wa mashindano ya umisenta na umishunta kitaifa mwaka huu bado wanaendelea na maandalizi mbalimbali ambapo leo wameanza kuandaa kiwanja ambacho kinategemewa kutumika katika mashindano ya mchezo wa mbio za riadha.
Akizungumza na michuzi kaimu Afisa michezo Mkoa wa Mtwara Mack Kayombo amesema kuwa maandalizi yanakwenda vizuri na wanategemea kuwa mchezo wa mbio za riadha mwaka huu utakuwa ni mchezo wa kwaza kuchezwa ikilinganisha na miaka iliyopita.
Kwaupande wake mkandarasi anaeandaa kiwanja hicho Johakim Makwiche amesema urefu wa kiwanja hicho ni mita 400 na anatarajia kukamilisha kazi ya kuandaa hapo kesho huku mwenyekiti wa chama cha mchezo wa mbio za riadha mkoa wa mtwara Omary NYENJE amesema wanatarajia ushindi katika mashindano ya mchezo huo.
Mkandarasi Johakim Makwiche anaeandaa kiwanja kinachotarajiwa kutumika katika mashindano ya umesenta kitaifa mchezo wa liadha chuo cha uwalimu( TTC)mkoani mtwara.(picha na Adam Juma)
Mkandarasi Johakim Makwiche anaeandaa kiwanja kinachotarajiwa kutumika katika mashindano ya umesenta kitaifa mchezo wa liadha chuo cha uwalimu( TTC)mkoani mtwara.(picha na Adam Juma)
kiwanja kinachotarajia kutumika katika mashindano ya umesenta kitaifa mchezo wa mbio za liadha chuo cha uwalimu (TTC) mkoani twara.(picha na Adam Juma)
shuguli za maandalizi ya uwanja unaotarajia kutumika katika mashindano ya mbio za liadha umeseta kitaifa chuo cha uwalimu mtwara (TTC).(picha na Adam Juma)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...