Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) amekutana na  kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bi. Natalie Boucly, ambaye amemaliza muda wa kuliwakilisha shirika hilo nchini. Katika mazungumzo hayo, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) alimshukuru Bi.Natalie Boucly kwa uwakilishi wake mzuri katika nyanja mbalimbali katika kuchochea maendeleo nchini.

Pamoja na mambo mengine, Prof. Palamagamba John Kabudi alimweleza Bi.Natalie Boucly ajisikie nyumbani na asisite kuitembelea tena Tanzania pamoja na vivutio mbalimbali vilivyopo nchini kama mbuga za wanyama na mlima Kilimanjaro pamoja na visiwa vya Zanzibar.  
Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akimsikiliza Bi. Natalie Boucly wakati wa mazungumzo hayo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe (wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Emmanuel Buhohela (wa pili kutoka kushoto), Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje Bw. Charles Joseph Mbando (wa kwanza kulia) pamoja Afisa Mambo ya Nje Bi Diana Mhina wakifuatilia kwa makini mazungumzo ya Prof. Palamagamba John Kabudi na Bi. Natalie Boucly (hawapo pichani)
Prof. Palamagamba John Kabudi akimkabidhi zawadi ya picha yenye mchoro wa vivutio vya utalii nchini Bi. Natalie Boucly.



Posted: 09 May 2019 04:58 AM PDT
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Vietnam hapa nchini Mhe. Nguyen Doanh (kushoto), mazungumzo hayo yamefanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Kitengo cha mawasiliano serikalini wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Emmanuel Buhohela (katikati), wa kwanza kulia ni Katibu wa Waziri Bw. Magabilo Murobi na Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Luangisha. E.F.L wakifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Palamagamba John Kabudi na  Balozi Doanh (hawapo pichani)
Mazungumzo yakiendelea
Prof. Palamagamba John Kabudi na Balozi Doanh wakiwa katika picha ya pamoja.



Posted: 09 May 2019 03:41 AM PDT
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya Mkutano wa SADC unaotarajiwa kufanyika hapa nchini mwezi August 2019,ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli anatarajia kupokea nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya hiyo na kutoa rai kwa Makampuni,taasisi za serikali na binafsi na wajasiriamali mbalimbali kuchangamkia fursa zitakazojitokeza wakati wa mkutano huo wa SADC.Mkutano huo wa waandishi wa habari umefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam.
Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari wakinukuu mazungumzo ya Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi kuhusu Mkutano wa 39 wa SADC utakaofanyika hapa Nchini mwezi August 2019 (hayupo pichani).
Sehemu ya wajumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na taasisi mbalimbali wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi na Waandishi wa Habari Kuhusu mkutano wa SADC utakaofanyika hapa Nchini mwezi August 2019.(hawapo pichani.)
Wapiga Picha wa Vyombo mbalimbali vya Habari wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi na waandishi wa Habari kuhusu mkutano wa 39 wa SADC kufanyika hapa Nchini mwezi August 2019.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...