Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme katikati akikata utepe kufungua soko la kuuzia Dhahabu na madini ya vito wilaya ya Tunduru kama utekelezaji wa agiza ka Rais Dkt John Magufuri aliloagiza kila wilaya na mkoa ambao una madini kufungua soko la kuuzia madini ambalo litawezesha wauzaji na wanunuzi kuuzia madini,wa pili kushoto ni MKuu wa Wilaya ya Namtumbo Mh.Sophia Kizigo.Picha na Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Ruvuma.
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi Christina Mndeme aliyenyoosha mkono akiongea na baadhi ya wanunuzi wa Madini waliosimama kushoto wakati wakati wa Ufunguzi wa soko la kuuzia Dhahabu na madini ya vito wilayani Tunduru,kulia ni Kaimu Mkuu wa wilaya ya Tunduru ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo.
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme katikati akipiga makofi jana mara baada ya kukata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa soko la kuuzia Dhahabu na madini ya vito katika wilaya ya Tunduru mkoani humo,wa kwanza kushoto mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru Mkwanda Sudi ,Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Sophia Kizigo na kulia Afisa madini Mkazi wa wilaya hiyo Juma Kapela.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...