Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
   
Ukisikia na ukifatilia unaweza ukaona kama jambo la kawaida tu katika kampeni hii ya Uzalendo kwanza inayongozwa na Steve Mangele Nyerere ambaye kwa kipawa ameweza kukusanya wasanii Zaidi ya 400 kutoka tasnia mbalimbali.

Nikiwa mkoani Tanga Wilaya ya Pangani wakati wa uzinduzi wa AWESO CUP, nilipata kusikia ushuhuda na matokeo ya ziara ya kundi hilo kwa mwaka jana katika Wilaya ya Pangani.

Ambapo moja ya jambo linalotajwa sana ni baada ya  kutoa msukumo wa kupatikana ujenzi wa barabara ya lami ya Tanga mpaka pangani.

Unaweza kujiuliza je wasanii wanaweza kujenga barabara mpaka useme ziara yao kuwa ilizaa matunda la hasha , lakini kutokana na umaharufu wao na wingi wa wafuasi katika mitandao ya kijamii waliweza kupaza sauti na kumshawishi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli ambapo aliagiza itangazwe tenda mara moja hili barabara hiyo ijengwe.

Juma Aweso ni Naibu Waziri wa Maji na Mbunge wa jimbo la pangani anathibitisha nguvu ya kundi hili mbele ya wakazi wa Wilaya ya Pangani.

Aweso anasema anawashukuru wakazi wa pangani kwa kumchangua yeye na kuwa mbunge wao na yeye amepata marafiki kutoka uzalendo kwanza ambao kwa sasa wanaisemea vyema wilaya ya pangani hatimaye kwa sasa Rais ameagiza barabara ya lami ijengwe kuanzia Tanga mpaka pangani.

“tulijaribu kwa nguvu zetu ikishindikana lakini kundi la uzalendo kwanza linaloongozwa na Steve Nyerere lilifika hapa Panagani mwaka jana kisha kuamua kuondoka na ajenda moja tu ya barabara ya Tanga pangani na hatimaye Rais wetu Msikivu Dr Magufuli amekubali kujenga bara bara hii kwa kiwango cha lami na mkandarasi ameagizwa aanze mara moja ifikapo mwezi wa tano”anasema Aweso.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Tanga Martin Shigella ambaye ndio alikuwa mgeni rasmi katika Tamasha hilo anakiri kupokea maelekezo kutoka ofisi ya Rais na kwa sasa barabara hiyo kuanza kujengwa mapema.

“taratibu za kutangaza tenda zilishaanza na tupo katika hatua za mwisho za kumpata mkandarasi atakayejenga barabara hii hivyo niwatoe shaka wakazi wa pangani kuwa ujenzi wa barabara hii utaanza mapema mwanzoni mwa mwezi May mwaka huu” amesema RC.Shigella  

RC. Shigella anasema katika ujenzi wa barabara hiyo watamuelekeza mkandarsi ujenzi uanzie pangani kwenda Tanga mjini kama mbunge wa jimbo hilo alivyoomba.
Akizingumza kwa niaba ya wananchi wa Pangani Mkuu wa Wilaya ya  Pangani, Zainab Abdalah anamshukuru kiongozi wa kundi la uzalendo kwanza na wasanii wote pamoja na wadau wengine waliofika pangani na kuendelea kuitangaza vyema wilaya hiyo.

Dc.Zainab anasema kuwa wapo wasanii lakini Steve Nyerere amekuwa na moyo wa kipekee na mzalendo kwa nchi yake kuliko vile wwatu wanavyofikiri.
Anasema kuwa sio jambo dogo kwa mtu kuweza kuwashawishi wasanii wenzio waweze kusafiri na kuja kujitolea kufanya hamasa katika wilaya ya pangani na kuacha raha na starehe zilizopo Dar es Salaam.
Anataja kuwa nchi ya marekani imekuwa ikipata umaharufu kutokana na wasaniii wan chi hiyo wanavyoweza kujivunia mambo yaliyopo nchini kwao hivyo Steve kupitia uzalen do kwanza amechagua njia iliyobora ya kuzungumzia kazi zinazofanya na rais wetu na kutoa hamasa kwa maeneo yaliyopo pembezoni kama pangani.
Akziungumza kwa niaba ya Wasanii wenzie Steve Nyerere ametaja kuwa upendo wa Wasanii kwa nchi yao ndio kitu pekee ambacho kinawafanya watoke kwenda sehemu kama hizo kutoa hamasa.

Anasema Wasanii wa kundi la uzalendo kwanza wametambua kuwa umaharufu wao umetokana na watu hivyo ni wakati wa wao kurudi kwa jamii kusema asante na kuwa daraj akw aajili ya kutatua matatizo yao.

“sio muda wote waytanzania wanatakiwa kuelezwa juu ya nchi yao kwa lugha ngumu kuna muda wanahitaji waambiwe kwa lugha nyepesi kupitia uwasilisho wa Sanaa na wanaelewa haraka na kuendelea kumuunga mkono Rais wetu Dk. John Pombe Magufuli” anasema Nyerere.

Anataja kuwa Rais Magufuli anamuda wa kuzunguka katika maeneo yote haya kuzungumza yaliyyotendeka lakini sisi kama wasanii wazelendo tunaweza kufika na kuwa sauti yake na ujumbe ukafika haraka sana.
 Mwenyekiti wa Kundi la Uzalendo Kwanza Steve Nyerere akizungumz ana wakzi wa Pangani
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shegella akikabidhi zawadi kwa Mwenyekiti wa Uzalendo kwanza Steve Nyerere

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...