Mwenyekiti wa Tasisi ya Tushikamane Foundation, Rosemary Mwapachu, akizungumza na wadau na Marafiki wa Taasisi hiyo waliofika katika hafla fupi ya kushukuru wafadhili walioiwezesha taasisi hiyo kujenga jengo la kulala wazee wasiojiweza huko Kwembe jijini Dar es salaam wakati wa hafla hiyo iliyofanyika mwishoni mwa juma hoteli ya New Africa jijini. Nyuma yake kushoto ni wanachama wa Tushikamane Foundation Bi. Anna Kahama na Mwami Mlangwa.
Jaji Mstaafu Mark Bomani akieleza na kutoa ushuhuda juu ya taasisi hiyo ilivyokuwa msaada kwa wazee na kutaja kuwa kitu wanachokifanya ni kikubwa zaidi kuliko watu wengine
Balozi Juma Mwapachu akimpongeza Mkewe Bi Rose Mwapachu kwa kufanya vizuri katika ujenzi wa nyumba ya Wazee na kufanikisha Harambee kwa ajili ya mahitaji ya wazee hao kwa mwezi
Sehemu ya Washiriki wa Harambee hiyo wakifuatilia kwa makini namna mambo yanavyoenedelea
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...