Na.Khadija seif,Globu ya jamii
MKAZI wa kata ya kilungule wilaya ya temeke jijini Dar es salaam Halima abdallah amewashauri wananchi kujijenga dhana ya kupima afya zao mara kwa mara ili kunusuru maisha yao .
Halima amesema kupitia huduma ya upimaji kwa hiari ilioandaliwa na madaktari wa kujitolea wa (TVMCS) ikishirikiana na diwani wa kata ya kilungule ameweza kubainika kuwa ana uvimbe tumboni.
"Huduma nilipatiwa bure na nikagundulika na uvimbe tumboni ambao ukiendelea kuwepo unaweza kuhatarisha maisha yangu, nawashukuru madaktari ambao baada ya kugundulika na tatizo hilo wapo bega kwa bega na mimi na wananipatia ushauri ,"
Hata hivyo kwa upande wa diwani wa kata ya kilungule Said fella amesema bado kuna changamoto kubwa kwa wananchi kujitokeza kwenye huduma za kijamii hasa kupima afya zao bure wengi wao hupuuza.
"Walijiandikisha wengi kupatiwa huduma hiyo takribani watu 500 lakini badala yake watu 372 ndio waliweza kufanya vipimo na kugundulika na magonjwa mbalimbali,"
Aidha,fella ameeleza kuwa tayari ameshaweza kuchangia madawa kwa magonjwa tofauti tofauti huku akiwataka wananchi kujijenga dhana ya kuwahi vituo vya afya kabla ya ugonjwa hujaleta athari kubwa zaidi.
Huku daktari kutoka (TVMCS) Issa Mohammed Nassor akiendelea kusisitiza wanatanzania wote kujikinga,kujilinda na kuepuka visababishi vya magonjwa mbalimbali ili kuimarisha afya zao.
Mohammed amebainisha magonjwa ambayo wananchi wamekuwa wakiishi nayo bila kujijua kama presha,kisukari ,uvimbe na kifua kikuu.
"Wagonjwa wapatao 182 waligundulika kuwa na tatizo la presha huku ,52 walikua na kisukari.
Pia Mohammed ameeleza yapo magonjwa ambayo yanatibika na hivyo wagonjwa wengine wameshaanza matibabu huku mgonjwa wa uvimbe tumboni Halima abdallah akifanyiwa maandalizi ya awali kwa ajili ya operesheni.
Diwani wa kata ya kilungule Said fella akitoa ripoti ya wakazi wa kata ya kilungule wilaya ya temeke jijini Dar es salaam waliojitokeza kupima afya zao katika huduma hiyo ya bure akishirikiana na madaktari wa kujitolea wa TVMCS.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...