Na.Vero Ignatus,Machame ,Kilimanjaro

Waziri mkuu wa Tanzania Kasimu Majaaliwa, ameongoza maelfu ya watanzania katika mazishi ya aliyekuwa mfanyabiashara maarufu  ukanda wa Afrika mashariki, Dr. Regnald Mengi, ambaye amezikwa leo katika makaburi ya familia nyumbani kwa wazazi wake kijiji cha Kisereni Machame mkoani Kilimanjaro Km 35 kutoka Moshi mjini.

Akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Waziri Mkuu Kassim Majaaliwa amesema kuwa taifa litamkumbuka Dkt. Mengi kwa mchango wake mkubwa wa kukuza uchumi nchini hasa katika sekta ya madini, habari, viwanda na mazingira, kwani amewahi kuwa mwenyekiti wa abaraza la mazingira Taifa.

 Waziri mkuu Majaaliwa amesema mchango wa Dkt.Mengi katika kuwakumbuka watu wenye mahitaji maalumu utaendelea kukumbukwa daima kuindokewa na mtu mzalendo katika historia ya Tanzania

"Hakuna Mtanzania asiyejua mchango alioutoa kwa Taifa hili,kwa namna alivyoguswa katika nyanja mbalimbali kwa jamii na hata kwa serikali, tunatambua mchango wake"alisema Majaliwa.

Amesema kuwa kama Taifa la Tanzania  msiba huo wa Dkt Reginald Mengi alikuwa ni mtu wa upendo na hakuwa na ubaguzi hivyo pigo na wameondokewa na mtu aliyekuwa muhimu maishani na Mungu alimbariki na yeye akawa baraka kwa wengine.

 Akitoa mahubiri katika ibada ya mazishi hayo iliyofanyika katika kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania KKKT Usharika wa Moshi mjini, Askofu mkuu wa Kanisa hilo Dkt. Fredrick Shoo, amewaasa viongozi wa serikali hasa wale wenye umri mdogo kuacha kiburi cha madaraka na badala yake watende haki kwa wananchi wote bila upendeleo na watapata za Mungu.

Dkt Shoo amemtaja Marehemu Mengi kuwa  hakuwabagua maskini japo alikuwa na tajiri na tabia hiyo inapaswa kuigwa na watu wote wenye nafasi za uongozi serikalini, wenye madaraka na wenye pesa.

Askofu Dkt. Shoo ameendelea kusisitiza kuwa kama Taifa la Tanzania linahitaji kupokea baraka kutoka kwa Mungu ni muhimu kuacha  ubaguzi,  kiburi na kujikweza,amekemea baadhi ya tabia ya kauli za viongozi ambazo zinaweza kuleta migogoro katika jamii.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzania nchini Tanzania Freeman Mbowe, amekemea tabia ya ubaguzi wa ukabila unaooneshwa na baadhi ya viongozi na kwamba ili kumuenzi Mengi ni muhimu kuyaacha matendo hayo kwani alikuwa ni mtu wa kujishusha japo alikuwa Bilione.

Katika hatua nyingine Askofu Dkt.Shoo amewataka Watanzania kuacha tabia ya kubaguana kwani ni dhambi mbele za Mungu ,wenye nafasi kuwakandamiza wale walio wa hali ya chini,amewataka kuacha kiburi 

"Hivi nyie viongozi haswa vijana mnapopata cheo mnajisahau wanaojitutumua kama chatu wakumbuke kuwa kila siku tunamuomba Mungu na lazima Mungu  atawashusaha"

Kwa upande wake Waziri mkuu Kassimu Majaliwa ametoa pole kwa familia ya Marehemu Dkt.Regnald Mengi kwa kuondokewa na mpendwa wao,amesema amepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya msiba wa Mengi

Tujifunze kuwathamini  watu wasio na uwezo katika jamii na Taifa kwa ujumla msikivu ,mpenda amani,na mwenye kuwasaidia wengine 1990 alianza kupata chakula cha pamoja na watu wenye ulemavu.

Kwa upande wake Mkuu CCM Taifa  Bashiru Ally amesema mchango wa Dkt. Mengi katika Taifa haswa katika mazingira  alisisitiza kupanda na kuotesha mingi tumuenzi na kupanda miti ya kutosha

"Baba Askofu hatujafanya kazi ya kuwaandaa vijana wetu kuwa Viongozi bora, sasa tunavuna matunda yake, naomba nimuombe msamaha kijana wangu Makonda, nilimsema Simiyu mara ya kwanza, akaja ofisini analia, ameanza kujirekebisha" alisema Bashiru

Akitoa salamu kwa niaba ya Bunge Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai amesema kuwa ameonyesha kwa hali na mali alikuwa na mali ila mkarimu na amefanya mengi ya heshima kubwa,alijitoa bila kujali alipanda miti zaidi ya milioni ishirini siyo jambo la kawaida.

"Nawaomba wananchi wenzangu msiamini kila kitu kinachoandikwa  kwenye mitandao ya kijamii ,vingine vya  uongo sana.alisema Ndugai

Kwa zaidi ya mzee mmengu ameshatangulia mbele za haki haitajalisha tutazungumza maneno mazuri kiasi gani ,tutakachoweza ni kuyaishi ya mema aliyotenda,alikuwa mnyenyekevu,kauli zake zilikuwa za kujenga,kupatanisha,mamlaka,fedha zinajenga kiburi zisipotumika vizuri,hakuwa kiongozi wa serikali 

Na hatimaye msafara ukafika katika kijiji cha Kisereni Machame mkoani Kilimanjaro,  ambapo ndipo mwili wa mfanyabiashara huyo maarufu umehifadhiwa katika nyumba yake ya milele. Eneo alilozikwa Dkt. Mengi ni eneo la makaburi ya familia ambapo pia wamezikwa wazazi wake na ndugu wengine.

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiweka shada la Maua kwenye Kaburi la Marehemu Dkt Reginald Mengi wakati wa mazishi,Machame mkoani Kilimanjaro

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...