Wamiliki wa shindano la Miss Utalii Tanzania , E.G.C .Honolulu Promotion ya jijini,ambayo ndiyo pekee yenye dhima ya kikomo ya haki za kuendesha na kusimamia shindano la Miss Utalii Tanzania tangu kuanzishwa kwake mwaka 2002, imeipa haki hizo taasisi ya Africa Tourism Promotion Centre. ambayo inajishughulisha na promosheni za utalii kimataifa, hususani barani Afrika.
Taasisi hiyo ya Africa Tourism Promotion Centre inaratibu pia uanzishwaji na ujenzi wa kituo cha kuratibu promosheni za vivutio vya utalii na utamaduni vya bara la Afrika, lakini pia inaratibu shindano la dunia la Miss Utalii Vyuo Vikuu (Miss Tourism University World), tuzo za utalii za Dunia,Afrika na Tanzania,Safari kuu ya utalii ya Dunia na Tanzania (World,Africa and Tanzania Tourism Awards),National Parks,Wildlife na Antpoaching International Marathons, World,Africa and Tanzania Tourism Life Party,na World,Africa and Tanzania Tourism Music Awards
Asante,
Geogina Saulo-Mkurugenzi wa Mashindano na uratibu
0769285645.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...