Na.Khadija seif,Globu ya jamii

MWAMITINDO Hamisa Mobeto ambae pia ni mwanamuziki chipukizi kwa sasa ameweka wazi kuwa hatoruhusu kukatishwa tamaa kwenye sanaa yake .
Mobeto ambae ameshafanya vibao mbali mbali Kama madam hero na kibao chake kipya alichomshirikisha msanii Christian Bella "Boss" anasema ataendelea kusimama na kukiamini kipaji chake cha kuimba.

" Sitazuia mtu kuongea kile anachokifiria na nitaendelea kusimama kwenye kile ninachokiamini siku zote na maoni yao kwa namna moja au nyingine zinani imarisha na kufanya niendelee kurekebisha baadhi ya makosa madogo madogo kwani bado sijawa na uzoefu wa kutosha Kama nilivo na uzoefu kwenye tasnia ya urembo na maigizo,"

Hata hivyo Mobeto ameeleza kuwa kufanya kazi na Msanii mkubwa Kama Bella ni nafasi kubwa Licha yakuwa mwanamuziki mzuri pia ni mwalimu mzuri katika muziki.Pia amesema ni mwanzo mzuri kufanya kazi na bella hivyo mashabiki zake wategemee vitu vingi vizuri.

Huku Msanii wa miondoko ya dansi nchini christin Bella amesema wazo la kufanya kazi pamoja lilitokea baada ya kukutana nchini Marekani ."Wakati nipo kwenye jukwaa nilimuita ili atumbuize wimbo wake wa madam hero ,"

Hata hivyo bella amesema amepokea baadhi ya maoni ya watu ambayo yamekua mengi ya kumkatisha tamaa mobetto." Hakuna mashindano wala bifu ni kazi tu tumeifanya kwa ajili ya mashabiki zetu waipokee nimeshaimba na watu tofauti Kama alikiba ,ommy dimpoz hivyo kufanya kazi na hamisa sio kitu kibaya japo wengi wamebeza sana ,"

Pia amemsifia mobetto kwa uwezo wake mzuri wa kushika mashairi kwa haraka zaidi .Hata hivyo Bella ameweka wazi kuwa mbali na kuachia kazi hiyo , mashabiki wasubiri vibao vingine vizuri kutoka kwa wawili hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...