Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, amewaongoza vijana wa rika mbalimbali katika mashindano ya mbio za Dassani Marathon KM 21, KM 10 na KM 05 zilizofanyika jijini Dar es salaam, huku wengine kadhaa wakijinyakulia zawadi kwa kuibuka washindi kwenye mbio hizo.
Akizungumza baada ya kukamilika kwa mashindano hayo ambapo IGP Sirro akiwa mgeni rasmi kwenye mashindano hayo pia alishiriki kwenye mbio za KM 10, IGP Sirro, amesema kuwa, suala la vijana kushiriki kwenye mashindano mbalimbali ya michezo kutasaidia kuwaepusha kujiingiza kwenye makundi ya kihalifu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...