Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula wa kwanza kushoto
na Kamishna wa Tume ya Madini Prof. Abdulkarim Mruma wa pili
kushoto, wakiwa kwenye mazungumzo na Mkuu wa Wilaya (DC) ya
Nachingwea Rukia Muwango wa kwanza kulia na kulia kwake ni
katibu tawala mkoa wa Lindi na Afisa madini mkazi mkoa wa Lindi
kushoto kwa RC.
Fundi Sanifu Mwandamizi Paulo Shauri wa kampuni ya Lindi Jumbo
katikati akionyesha na kutoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Tume ya
Madini Prof. Kikula kulia kwake na Kamishna wa Tume ya Madini
Prof. Abdulkarim Mruma kushoto kwake kuhusu muundo na
muonekano wake pindi utakapo anza kufanya kazi hapo mwakani
mwezi August 2020.




Na Issa Mtuwa (Wizara ya Madini) Rwangwa.

Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula na Kamishna wa Tume
hiyo Prof. Abdulkarim Mruma wamefurahishwa na mgodi wa Namungo kwa
namna unavyofanya kazi zake kwa utaratibu na mpangilio kiasi cha
kutamka kuwa wanatamani migodi mbalimbali iende ikajifunze mgodini
hapo.

Hatua hiyo inafuatia ziara waliyoifanya mgodi hapo kujionea uendeshaji wa
shuguli za mgodi huo sambamba na kukagua na kusikiliza kero kutoka kwa
wachimbaji wadogo, wakubwa na kati.
Wakiwa mgodini hapo wameupongeza mgodi huo kwa namna
wanavyowashirikisha wachimbaji wadogo na kuwapa umiliki wa 83% ya
mapato yanayotokana na uzalishaji huku mgodi ukibakiwa na 17% ya
kinacho zalishwa kitu ambacho hawajakikuta kwenye mgodi wowote hapa
nchini.

Kutokana ushirikishaji wa wachimbaji wadogo, mgodi huo umekuwa ni
wautofauti na migodi mingine kwani hakuna malalamiko hata kidogo kutoka
kwa wachimbaji wadogo tofauti na maeneo mengine nchini ambapo
kumekuwa na mivutano kati ya wachimbaji wadogo na wachimbaji wa kati
na wakubwa.

“Niseme ukweli nimefika hapa nikiwa nimechoka na safari ndefu, lakini
mara baada ya kupokea taarifa hii na kuwaona wahusika na hawajabisha
kuhusu taarifa hii, kwa kweli nimepata nguvu sana, nyie ni mfano wa
kuigwa, hiki mnachokifanya hakifanywi maeneo mengine sisi tunazunguka
nchi nzima lakini nyie mnafanya kitu cha kipekee” amesema Prof. Kikula.

Aidha, wameupongeza mgodi kwa ulipaji wa maduhuli ya serikali kama
inavyotakiwa huku akiwapongeza kwa utekelezaji wa shuguli za
maendeleo ya jamii (Corporate Social Responsibility- CSR).

Akiwasilisha taarifa yake kwa mwenyekiti wa tume ya madini, Meneja wa
mgodi wa Namungo Alfred Kimbi amesema kwa kipindi cha January –
December 2018 mgodi huo ulizalisha gramu 54,920.30 yenye thamani ya
Tshs. bilioni 4.302 na kuwawezesha kulipa mrabaha wa jumla ya Tshs.
milioni 412,607,105, huduma za jamii (service levy) Tshs. milioni
19,290,596 mamlaka ya mapato (TRA) Tshs. milioni 156,577,270. Kwa
mwaka 2019 kuanzia Januari hadi Mei mgodi umezalisha dhahabu gramu
16,671.5 yenye thamani ya jumla ya Tshs. bilioni 1.423 nakufanikiwa kulipa
mrabaha na ada ya ukaguzi kiasi cha Tshs. milioni 99,599, 450.61, mgodi
pia umelipa kwa TRA kiasi cha Tshs. milioni 51,142,000 katika kipindi
hicho.

Kimbi ameongeza kuwa pamoja na ulipaji wa tozo hizo, kwa mwaka huu
2019 mgodi pia umelipa kodi nyingine kama vile kodi ya Mazingira milioni
5,000,000 Osha milioni 3,800,000 na ushuru wa Halmashauri milioni
21,880,990.

Kuhusu utekelezaji wa shuguli za maendeleo ya jamii, mgodi wa Namungo
umetekeleza mirandi mbalimbali ya Elimu kwa baadhi ya shule ikiwa ni
pamoja na kulipa walimu na wafanyakazi wengine, ujenzi wa madarasa ,
umefadhili ujenzi wa kisima cha maji katika kijiji cha Chingubwa chenye
thamani ya Tshs. Milioni 13,000,000. Kwa upande wa afya mgodi
unaendelea kutekeleza mradi wa ujenzi wa Zahanati katika kijiji cha
Chingumbwa mradi ambao utagharimu Tshs. 90,594,800. Kuhusu michezo mgodi umeshiriki kikamilifu kiasi cha kuiwezesha timu iliyopewa jina la
mgodi huo “Namungo Football Club” kupanda daraja kufikia Ligi kuu kwa
msimu ujao 2019/20.

Ziara hiyo iliyoanza tarehe 8/6/2019 katika mikoa ya Lindi na Mtwara leo
10/6/2019 iliendelea katika wilaya ya Nachingwea kwa Mwenyekiti na
Kamishna kuzungumza na wafanyakazi wa tume hiyo mkoa wa Lindi
kwenye ofisi za tume hiyo zilizopo Wilayani Nachingwea na baadae
kufanya mazungumzo na Mkuu wa Wilaya hiyo Rukia Muwango kisha
kuelekea wilaya ya Rwangwa ambapo walitembelea Soko la Madini, eneo
la kampuni ya Ngwena Tanzania Ltd “Ngwena” inayojishugulisha na
shuguli za utafiti wa madini ya Graphite na baadae kwenye kampuni ya
Lindi Jumbo pia inayojishugulisha na uchimbaji wa madini ya Graphite yote
ikiwa wilaya ya Rwangwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...