Na.Vero Ignatus,Arumeru.

Mwenge wa uhuru umezindua miradi yenye thamani ya shilingi Bilioni 22.9 na miradi I6 katika sekta ya kiliko,afya,maji ,kilimo,ufugaji kwenye halmashauri zote mbili za Arusha DC na Meru.

Licha ya mwenge huo kuzindua miradi hiyo bado kumekuwa na changamoto katika baadhi ya miradi ambayo imetembelewa ambapo Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro ameahidi kusimamia kuhajikisha changamoto hizo zinanalizika kabisa.

Muro ameyaeleza hayo mapema jana wakati akikabidhi mwenge huo wa uhuru kwa mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro eneo la Moivaro jijini Arusha.

Hata hivyo ameeleza kuwa kati ya miradi 16 mradi iliyozinduliwa na mwenge huo, mradi mmoja wa Maji ambao ulianza kutekelezwa mwaka 2017 umekuwa na changamoto kutokana na wahusika kutofanya kazi kama inavyotakiwa katika mradi huo.

"Mwenge wa mwaka huu ni wa kweli kweli hauna mchezo na ukikuta kuna changamoto yeyote unaelimisha na kuelezwa namna ya kuitatua na pale walipofanya vizuri mwenge unawapongeza" Alisema Muro.

Akipokea mwenge huo ,mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro, amesema mwenge huo utakagua,kuzindua,kuweka mawe ya msingi kwenye miradi 8 yenye thamani ya shilingi bilioni 521 ambayo inahusisha,afya elimu, maji ,mazingira na ujasriamali .

auli mbiu ya mwaka huu ni Maji ni haki ya kila mtu tutunze vyanzo vyake ,tukumbuke kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa.Mwenge huo kesho utakabishiwa wilayani Monduli na siku inayofuata utakabidhiwa wiolayani Karatu ambapo utahitimisha mbio zake mkoani Arusha na kukabidhiwa mkoani Manyara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...