
Wabunge hao wamepata nafasi ya kuzungumza na wachezaji pamoja na viongozi waliopo na kambi hiyo nchini Misri,kwa leongo la kuweza kuwapa hamsa katika kuelekea mchezo wao wa kwanza wa tangulizi dhid ya Senegal na michezo mingine inayofuatia.
Mbunge wa Viti Maalumu,Mheshimiwa Salma Kikwete,akizungumza leo kwa niaba ya wabunge wengine alisema:
“Napenda kuwapongeza sana kwa kazi kubwa na nzuri kuanzia mwanzo na hatimaye kesho tunafikia kileleni,tumekuja hapa kwa ajili ya kuungana na timu kuwatia moyo na kuwatia shime na kuwaambia kwamba tumekuja Misri sio kushiriki bali kushinda,”alisema na kuongeza:
“Ushirikiano katika timu yaani ‘team work’ ndiyo itakayoleta ushindi,kwa maana hiyo Watanzania wote macho na masikio yao ni kwenu, kwahiyo,mtangulizeni Mwenyezi Mungu na Mungu atawasaidia.”
Kwa upande wa Mheshimiwa Magreth Sitta alisema, ”Nawapongeza sana vijana ambao wamechaguliwa katika hii timu,siku zote mi huwa napenda kuchukua mfano wa Leicester City ya England,wakati inachukua ubingwa haikuwa na mchezaji hata mmoja ambaye anajulikana sana,lakini waliweza kupambana kwahiyo na nyie msigope majina naamini mnaweza.”
Wabunge hao walifunga mazungumzo yao kwa sala ya pamoja na wa chezaji na viongozi,kwa sala iliyoongozwa Mheshimiwa Mchungaji Peter Msigwa,kwa ajili ya kuiombea timu ya taifa katika mchezo wa kesho na michezo mengine miwili dhid ya Kenya na Algeria.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...