Joseph Mpangala 

Wakulima wa korosho mkoani Mtwara wametakiwa kuacha Kujibweteka na badala yake wawatumie wataalamu ili kufanya kilimo cha tija kwa kutumia viuatilifu kwa usahihi na kupanda miche mipya 

kulima Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa amewataka wakulima wa korosho mkoani humo kuacha kujibweteka na kuwatumia wataalamu wa kilimo Sam namba na kupanda miche mipya ya kisasa iliyofanyiwa utafiti ili kuendana na ushindani wa mikoa mipya inayoanza kuzalisha zao hilo.

Akifungua rasmi mafunzo ya matumizi sahihi ya viuatilifu kwa baadhi ya wakulima wa korosho na maafisa ugani katika kijiji cha Mailikumi mkoani humo ambayo yatafanyika katika mikoa yote inayolima korosho amesema mikoa mipya iliyoingia katika kilimo cha korosho wanalima kisasa na matumizi sahihi ya viuatilifu.

“Tunavyojisifu na kuendelea kutamba kwamba sisi ndio wazalishaji wakubwa ip mikoa mingine ambayo imeanzisha uzalishaji, sasa tukiendelea kubweteka sisi ndio wazalishaji wakubwawenzetu huko wanalima kisasa na wana matumizi sahihi ya viuatilifu na tukibweteka tutajikuta tuko nyuma na wao watazalisha kwa wingi zaidi.

Amesema asilima 60 ya korosho inalimwa Mtwara wakiguatiwa kwa karibu na mikoa ya Lindi na Ruvuma na kwamba mikoa mingine wana maeneo mengi ya kulima.

“Wenzetu bado wana maeneo na pengine kutumia mbegu za kisasa zilizotokana na utafiti wa chuo cha Naliendele, mwisho wa siku tutapoteza ushindani, wanamtwara siku za usoni takwimu za uzalishaji zinaweza kubadilika mkajikuta nyie ni wa mwisho,”amesema Byakanwa

Kaimu mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho, Francis Alfred amesema Kama tasnia ya korosho wanaangalia kuanzia uzalishaji mpaka masoko hivyo wameanzisha mafunzo kwa wakulima ili kuongeza uzalishaji.

“Kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita 2017/18 uzalishaji ulipanda ukawa tani 313,000 lakini mwaka tunaomalizia 2018/19 uzalishaji umekuwa tani 244,000, sasa sisi jukumu letu ni kuhakikishana Marika kwamba uzalishaji unapanda tukaona ni lazima kuandaa mafunzo kwa wakaulima naMarika maafisa ugani yatakayofanyika katika mikoa yote inayozalisha korosho,”amesema Alfred

Akizungumza mkuu wa Teknolojia,unyunyuziaji wa viuatilifu TPRA,Mhandisi Julius Mkenda amesema baadhi ya dawa ambazo hazina lugha rafiki zimekuwaWaikiki's zikiingizwa nchini lakini kwa kupambana kwa asilimia kubwa vimepungua.
Kuliko.

Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dk Fortunatus Kapinga amesema wamekuwa wakiendelea kutoa mafunzo kwa wakulima namna ya kutambua magonjwa na matumizi sahihi ya viuatilifu.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...