Na, Editha Edward-Tabora
Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini Mhe, Emmanuel Mwakasaka amefanya Ziara ya kukutana na Wananchi ikiwa ni pamoja na kutoa Mrejesho juu ya Uwakilishi wake katika bunge
Katika Ziara hiyo Mwakasaka ametekeleza ahadi zake kwa wananchi wa kata ya Malolo alizoahidi hapo nyuma Mwakasaka amewawezesha kikundi cha wanawake kilichopo kata ya Malolo kwa kuwapatia kiasi cha fedha cha Sh. 500,000 kwa ajili ya kufanya shughuli za ujasiriamali
Pia amewawezesha vijana wa kata ya Malolo welding kwa kuwapatia Mashine kwa ajili ya kufanya shughuli za uchomeleaji ili waweze kujipatia kipato, na ametoa vifaa vya michezo kwa timu ya wavulana ya kata ya Malolo kwa kuwapatia mipira Miwili, Filimbi, pamoja na pump ya kujazia mipira
Kwa hatua nyingine madereva wa Tax wapatao 36 wamejiunga na chama Cha Mapinduzi CCM ili kumuunga mkono Mhe, Mwakasaka kwa Kazi kubwa anayoendelea kuifanya Tabora Mjini
Aidha Mwakasaka amewataka wananchi hususani kikundi cha wanawake pamoja na vijana kutumia msaada huo katika kujikwamua kiuchumi na kuwataka wafanye Kazi Ili kusaidia jamii ya watu wengine wa familia zao kwa ujumla pia Ziara hiyo imeqmbatana na naibu Waziri Eng.Nditiye Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi mawasiliano.
Pichani ni mbunge wa Jimbo la Tabora mjini Mhe, Emmanuel Mwakasaka akiwakabidhi Wanawake Wa kata ya Malolo Fedha.
Pichani ni vijana wa kata ya Malolo wakiwa wamebeba vifaa vya michezo walivyopatiwa na mbunge Mwakasaka.
Mbunge Emmanuel akizungumza na Wananchi wa Kata ya Malolo Mkoani Tabora.
Mbunge Mwakasaka akisalimiana na baadhi ya vijana wa kata ya Malolo waliojiunga na Chama Cha CCM.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...