Na Amisa Mussa
JESHI LA POLISI MKOANI TABORA KWA KUSHIRIKIANA NA KAMATI MAALUMU  KUTOKA MIKOA YA SHINYANGA NA TABORA  AMBAYO IMEHUSISHA VYOMBO MBALIMBALI  VYA ULINZI NA USALAMA IKIWEMO BODI YA SUKARI ,WATAALAMU KUTOKA  KIWANDA CHA SUKARI KILOMBERO PAMOJA NA WATAALAMU WENGINE KUTOKA TAASISI ZA  TFDA, TRA, WAKALA WA VIPIMO NA OFISI YA MKURUGENZI WAMEENDESHA OPERATION  MAALUMU YA  KUKAGUA BIDHAA MBALIMBALI ZA CHAKULA HUKO MKOANI TABORA NA KUFANIKIWA KUWAKAMATA WAFANYABIASHARA WATANO WAKIWA NA VIFUNGASHIO  MBALIMBALI VYA BIDHAA AMBAVYO SI HALISI (FAKE) .
Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Tabora Kamishna Msaidizi Wa Jeshi La Polisi  EMMANUEL NLEY Anasema Wafanyabiashara Hao  Watano Ambao Kwa Sasa Wote Wapo Mikononi Mwa Jeshi La Polisi Mkoani  Humo Wamekua Wakibadilisha  Kwenye Vifungashio Sukari Ya Kiwanda Cha Kutoka Nje Ya Nchi Na Kuiweka Kwenye Mifuko Ya Kiwanda Cha Kilombero Ili Waweze Kuuza Kwa Bie Ya Juu Huku Wakipunguza Ujazo Wa Mafuta Kwenye Bidhaa Ya Mafuta Ya Korie Lita Moja Kwa Kila Lita Ishirini Wakitafuta Faida
Wakati Huohuo KAMANDA NLEY Amesema Watu Wanne Wanashikiliwa Na Jeshi La Polisi Wakiwemo Watumishi Wawili Wa  Bohari Ya Dawa  Mkoa Wa Tabora Msd Kwa Tuhuma Za Kuiba Dawa  Aina Ya ALU Maarufu Dawa Mseto Wakidaiwa Walikua Wakisafirisha Kupeleka Nchi Jirani
Aidha KAMANDA NLEY Amebainisha Kuwa Watuhumiwa Wote Ambao Kwa Sasa Wapo Mikononi Mwa Polisi Watafikishwa Mahakamani Mara Baada Ya Upelelezi Kukamilika.
 SEHEMU YA SHEHENA YA DAWA ALMAARUFU KAMA DAWA MSETO
 KAMANDA WA POLISI MKOA TABORA ACP EMMANUEL NLEY
VIFUNGASHIO MBALIMBALI VYA BIDHAA AMBAVYO SI HALISI(FAKE)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...