Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Elinimo Shang’a
akielezea majanga ya moto yanavyotokea na namna ya kukabili.
Kamanda Shang’a akifundisha kwa vitendo namna ya kuzima moto kwa
kutumia blanket maalum ya kuzimia moto (fire blanket).
Kamanda Shang’a akielekeza namna ya kuzima moto kwa kutumia
kizimia moto aina ya poda kavu (dry powder fire extinguisher).
Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Mloganzila wakifanya zoezi
la kuzima moto mara baada ya kupatiwa mafunzo ya kinga na tahadhari dhidi yamajanga ya moto.
Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Peter Mwambene
(kushoto) akiwapatiwa mafunzo ya kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya motowatumishi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, kulia ni MkaguziMsaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Elinimo Shang’a.
Watumishi wa Hospitali ya Mloganzila wakifuatilia mafunzo hayo.


Dar es salaam 24-07-2019

Wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila wamepatiwa mafunzoya kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto kwa lengo la kujikinga namajanga ya moto na kuhakikisha Tanzania inakua salama dhidi ya majanga yamoto.

Mafunzo hayo ya siku mbili ambayo ni yanadharia na vitendo yametolewa na Jeshila Zimamoto na Uokoaji.Akizungumza katika mafunzo hayo Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto naUokoaji Peter Mwambene amesema moja ya vitu vinavyomfanya mtu ashindwekupambana na moto ni uoga na kutokua na vifaa sahihi vya kupambana na motounapokua katika hatua za awali.

Hivyo mafunzo hayo yatawajengea uelewa wa matumizi sahihi ya vifaa vya
kuzimia moto, kujua aina mbalimbali za moto na namna ya kukabili, kujua mbinuza kuzima moto pamoja na namna ya kujiokoa pindi moto unapotokea.
“Moto unapotokea mtu hushindwa kuukabili kutokana na uoga, unatakiwa ufanyeyafuatayo pindi unapogundua moto, piga king’ora, kengele au mayowe,ita Jeshi laZimamoto na Uokoaji kupitia namba 114, watu wasiojiweza wapewe kipaumbelekutoka eneo hatarishi, jaribu kuzima moto bila kuhatarisha usalama wako na watuwengine’’ amesema Mwambene.

Ametaja vyanzo vikuu vinavyoweza kusababisha majanga ya moto kuwa ni
matumizi ya vifaa vya umeme visivyokua na ubora, ajali, nguvu asilia (radi,
upepo,mkali, tetemeko la ardhi , milipuko ya Volkano).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...